Skip to main content

SABABU ZINAZOCHANGIA WATU KUSHINDWA KUFIKIA MALENGO YAO

TUNAWEKA MALENGO SAWA NA HATUFANIKIWI SAWA, NINI SABABU YA WATU KUSHINDWA KUYAFIKIA MALENGO YAO
Duniani kote kila mwishoni au mwanzoni mwa mwaka watu hupanga Malengo mengi sana, tena hupanga Malengo mazuri, ukiyaangalia unaona mafanikio makubwa mbele yao. Na umekuwa ni Utamaduni uliozoweleka sana watu kupanga Malengo kila mwishoni na mwanzoni mwa mwaka.
Kwa mujibu wa takwimu Bubu inaonyesha kwamba katika kila watu million moja ambao huweka Malengo, nusu yake huwa wanasahau kabisa ifikapo mwezi machi na robo 3 huishia kusingizia changamoto zinazowazunguka na 1/3 yake ndo huyafikia malengo yao.

HEBU TUANGALIE NI SABABU ZIPI ZINAZOCHANGIA HALI HII????
ü        Kukosa nidhamu ya matumizi ya pesa na muda. Utajiri wa kwanza duniani ni matumizi mazuri ya muda/wakati, ukitumia muda na pesa vibaya huwezi kuyafikia malengo yako.
ü        Aaina ya marafiki ulionao,     inayoweza kukufanya ushindwe kuyafikia mafanikio yako ni marafiki, hapa nazungumzia marafiki wasiokuwa na tija kwako, ukiendekeza kuwapa nafasi marafiki kuchezea Malengo yako huwezi kusonga mbele. Sisemi usiwe na marafiki, uwe na marafiki wenye ushawishi na ndoto zako. 
ü        Kukosekana kwa Maarifa na taarifa muhimu kuhusu Malengo yako, siku zote unapoweka Malengo yako, jitahidi kutafuta Maarifa na taarifa zinazoendena na Malengo yako. 
ü        Kukimbilia kila fursa inayojitokeza mbele yako huku ukisahau Malengo yako. Siyo fursa zote zinazokuja kwako zaweza kuwa na faida kwako, kinachotakiwa ni wewe kuzichunguza fursa na kuona katika zinawezekana kwako. Lakini pia fursa mpya zisikuharibie malengo na ndoto zako.
ü        Changamoto za afya na elimu, unapoweka Malengo yako huku ukisahau kuitunza afya yako utaishia kuutumia muda wa kutekeleza mipango yako kutibu afya, unapoweka Malengo yako, pia hakikisha unajali afya yako. Pi elimu, unapoweka Malengo yako usisahau kujiendeleza kielimu ili uendane na mabadiliko yanayoikumba duniani kisayansi na kiteknolojia.
ü        visingizio, ukiwa ni mtu wa kupenda kusingizia mambo mbalimbali huwezi kufanikiwa katika kuyafikia Malengo yako
KWA MFANO
u      Sina elimu
u      Rais kabana
u      Wazazi wangu hawakuniwekea msingi
u      Serikali hainijali
u      Ndugu zangu hawanipendi
u      Sina hela.
ü        Kukosa uthubutu, unaweza kuweka mipango mizuri sana lakini ukakosa nguvu ya uthubutu yaani nguvu ya kujaribu kufanya.
ü        Tamaa ya kutaka kufanya kila kitu bila kuweka vipaumbele katika malengo yako
ü         uvivu, Uoga na kutokujitambua, lazima ujitambue kuwa wewe ni wa pekee Sana na lazima ujue kama hutafanya wewe hakuna mwingine wa kufanya.


Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi