Skip to main content

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA

WITO NI NINI?
Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.
 Wito: Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo.

NITAJUAJE NIMEITWA?
1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani.MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama utajiita kwenye utumishi,tulia umsikie Mungu akisema na wewe na kukuelekeza nini cha kufanya kaika wito aliokuitia. “Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.”KUTOKA 3:4
SAMWELI
“basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.Kwa hivyo Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia.”1SAMWELI 3:4-10Hapa tunaona umuhimu wa kuitambua sauti ya Mungu.Yamkini Mungu amekuwa akikuita kwa ajili ya utumishi lakini umekuwa ukisita ukifikiri ni akili na mawazo yako  na umeshindwa kuitikia wito kama Samweli kabla hajaijua sauti ya Mungu.Lakini baada ya kuijua sauti ya Bwana Samweli aliitika.
YAKOBO
Mungu kabla ya kumtuma mtu katika utumishi wowote uanza na kumwita mtu huyo.Hata mzee Yakobo/Israel  alipoambiwa na Mungu ashuke Misri,Mungu alisema nae kwa njia ya ndoto.Hata wewe Mungu atakuita kama bado haupo kwenye utumishi.“Mungu akanena na Israeli katika ndoto ya usiku, akasema, Yakobo, Yakobo. Akasema, Mimi hapa.”YAKOBO 46:2
2.Mungu akikuita atjitambulisha kwako:Kabla ya kuingia kwenye wito wowote jitahidi kujua ni nani aliyekuita kwenye wito huo.Kuna watu wanatumika wakidhani wanamtumikia Mungu kumbe siyo Mungu bali miungu.Wengine wanatumika lakini hawafahamu ni nani wanayemtumikia.Mfano Musa alipo itwa Mungu alijitambulisha kwake “Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.”KUTOKA 3:6
3.Mungu atakuambia cha kufanya:Katika  maisha ya kawaida hata mzazi akimwita mtoto wake umwambia cha kufanya.Hata sisi Mungu anapoweka wito wa kazi yake ndani ya mioyo yetu utuelekeza tufanye nini.Musa aliambiwa awaokoe watu wa Mungu “Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”KUTOKA 3:10

Asante sana msomaji wangu kwa kuendelea kujifunza..Somo letu litaendelea tena wiki ijayo.Mungu akubariki

Subira Mlaga
Mwl,Mwandishi naMzungumzaji
Simu:0672745219
Barua pepe:subira.mlaga@yahoo..com





Comments

  1. Nimebarikiwa Sana ila Kuna wakati mwingine huwezi sikia saut Kama ya msa nasikiaga msukumo hiyo ikoje?

    ReplyDelete
  2. Je na kufanya kazi ya serikali ni wito au ni utandawazi wa kijamii

    ReplyDelete
  3. Iyoo nikazi tofautisha wito na kazi

    ReplyDelete
  4. Ubarikiwe mtumishi wa Mungu ila akuna Yakobo 46

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi