Skip to main content

SABABU ZINAZOPELEKEA FIKRA ZA VIJANA WENGI KUWA HASI


    SABABU ZINAZOPELEKEA FIKRA ZA VIJANA WENGI  KUWA HASI
MWANDISHI JOAS YUNUS JYB
Kadri binadamu anavyokua anakutana na mazingira mbalimbali .Mazingira ni pamoja na watu tunaokutana nao, vitabu tunavyosoma, mambo tunayoyaona na kusikia. Mazingira huanza kuathiri mtazamo wa kijana wa kuzaliwa nao na kwa bahati mbaya vijana wengi mtazamo wao chanya hubadilika na kuwa mtazamo hasi.

Mtu anapokuwa mdogo anapenda kufika mahali fulani lakini kadri anavyoendelea mbele, ndoto zake huanza kuyeyuka kutokana na watu anaokutana nao pamoja na vitu anavyosikia ambavyo hubadili mtazamo wake kutoka chanya kwenda hasi. Wachache wanaokutana na mazingira sahihi ndio hao hufikia ndoto zao na kuwa na mafanikio makubwa.
Zipo sababu kadha wa kadha zinazosababisha mtu kuwa na fikra hasi. Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na:

·         Marafiki
Vijana wengi wameshindwa kujua kuwa maisha tunayoishi na tutakaoishi yanatokana na watu wanaotuzunguka.Kama unazungukwa na watu wenye mtazamo hasi basi hata wewe utakuwa hivyo hivyo. Vijana wengi sasa wameshindwa kuwa na jicho la tatu la kujua nani na kwanini anapaswa kuwa rafiki yake. Unapokuwa umezungukwa na watu wanaomini kuwa mafanikio ni ajali, mafanikio ni bahati, mafanikio ni kwa baadhi ya familia ni lazima mtazamo wako uanze kuamini vitu hasi.

o   Vitabu
“Kimuingiacho mtu ndicho kimtokacho”. Ukweli ni kwamba vitabu tunavyosoma vina athari kubwa kwenye maisha yetu. Watu wengi wamekuwa wasomaji wa vitu ambavyo haviwajengi. Vijana wengi hupenda vitabu vya udaku kuliko vitabu vya kuwaletea maendeleo yao na vinavyojenga maadili.
Ubongo wako ni kama tumbo lako linalohitaji kula kila siku. Kama tumbo likiingiliwa na kitu kibaya huathirika. Hata ubongo pia unapokuwa umepata vitu vibaya huathirika vivyo hivyo.

o   Vitu tunavyosikiliza na kuangalia.
Runinga zetu na redio zetu zina athari kubwa kwenye maisha yetu ya kila siku. Vijana wamekuwa wakisikiliza na kuangalia sana nyimbo za kuamsha mapenzi kwa muda mwingi badala ya kusikiliza vitu vya msingi vya kujenga maisha yao.
Unaposikiliza au kuangalia kitu kwa muda mrefu kinakaa akilini na kuathiri sehemu ya ubongo. Unapotumia muda mwingi kusikiliza vitu vibaya maana yake sehemu kubwa ya ubongo wako ambao ndio huratibu maisha yako utakaliwa na vitu vibaya visivyo na tija.

o   Mfumo wa Elimu yetu:
Mfumo wa elimu pia umesababisha kuwajenga watu kuwa na mitazamo hasi ya kuamini kuajiriwa kuliko kutumia uwezo ulioko ndani yao katika kuzalisha na kutengeneza ajira zao binafsi na za watu wengine .
Siku moja nikiwa nasoma chuo kikuu cha Dar es salaam sehemu ya Mlimani, mhadhiri aliongea neno moja ambalo lilinishangaza mhadhiri alisema maneno haya “Ukimaliza chuo hiki si rahisi kukosa ajira” maana yake kwamba mhadhiri anaamini katika kuajiriwa tu. Nilitegemea mhadhiri angesema maneno haya “Ukimaliza chuo hiki unao uwezo wa kuwa na kampuni yako na taasisi yako”. Msemo wa hadhiri  ulinionesha wazi kuwa elimu tunayosoma darasani haituandai sana kusimamia shughuli zetu binafsi.
Naomba nieleweke  kwamba kuajiriwa si  kubaya lakini kibaya ni kuwajenga watu katika mitazamo ya kuajiriwa tu wakati wana uwezo mkubwa wa kujiajiiri .

o   Mapokeo

Vijana wengi huamini katika kile walichokikuta katika familia zao, nchi yao n.k. Huamini kuwa maisha ni bahati na nyota jambo ambalo si sahihi.Vijana huamini kama maisha tunayoishi yanatokana na historia ya familia zetu jambo ambalo siyo kweli .Kuzaliwa kwenye familia maskini siyo kigezo cha wewe kufa maskini .Hatuwezi kuchagua tuzaliwe katika familia yenye hadhi gani lakini tunaweza kuamua tufe tukiwa na familia za hadhi gani.

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi