Skip to main content

MAMBO YA KUZINGATIA KUFIKIA MALENGO YAKO

UKITAKA MAMBO YAKO YAENDE VIZURI KATIKA MALENGO ULIYOJIWEKEA FANYA MAMBO YAFUATAYO ;

A) Imarisha na kujenga mawasiliona mazuri na mahusiano mazuri pia kati yako na watu wanaokuzunguka. Kama ni malengo ya kibiashara jitahidi kuwa na mawasiliona mazuri na wateja wako. Ili kukuza mawasiliona jitengenezee kitu kinaitwa “business cards" yenye mawasiliona yako yote muhimu yaani namba ya simu, email na hata website kama ipo.

B) Jijengee tabia ya kutumia vizuri muda (wakati), kwa lugha nyepesi unaweza kusema zingatia sana muda wako na ikiwezekana panga ratiba yako mapema. Usipoteze muda wako kwa vitu visivyokuwa vya msingi wowote katika maisha yako. Kila kukicha jiulize nitafanya nini Leo? Na nitaanza na nini?? Na kumalizia saa ngapi???. Muda ni mali usipoutumia vizuri utaisha bila kufanya kitu.

C) Jiamini na kujidai mbele ya maadui zako, hapa namaanisha usiogope changamoto zilizopo katika kile unachotaka kukifanya. Kumbuka Uoga ni adui wa mafanikio yako. Pia Uoga ni udhaifu na ni dhambi kwa watu wanao Amini. Mtu asiyejiamini ni ngumu sana kufanikiwa katika maisha yake.

D) Uwe na nidhamu na heshima kwa watu wote bila kujali umri, hadhi au madaraka au muonekano. Usimdharau mtu yeyote. Mtu mwenye nidhamu na heshima ni mtu mwenye  hekima pia. Mtu mwenye hekima kichwa chake hujaa Maarifa na utayari wa kujifunza mambo mengi kuhusu maisha na kazi yake.

E) Uwe mwaminifu na mkweli, ukitaka kufanikiwa katika maisha yako jijengee tabia ya uaminifu na kuwa mkweli, hapa pia jifunze kuwa na siri na kutimiza ahadi zako. Kwa mfano kikao ni saa kumi jioni wewe unakuja saa moja jioni, umekosa uaminifu na hujawa mkweli na umeshindwa kutimiza ahadi yako.

F) Uwe na lugha ya ushawishi kwa shughuli au malengo yako. Unaweza kuwa na jambo zuri lenye kuleta tija kwako na kwa Jamii nzima, lakini ukakosa nguvu ya ushawishi. Mtu mwenye lugha ya ushawishi kwa biashara au huduma yake atapata wateja na walaji wa bidha au huduma yake zaidi.

G) Jifunze kuwa mtu wa kutoa maamuzi usipende kila kitu kiamliwe na watu wengine. Jijengea tabia ya kuamua juu ya hatima ya maisha yako.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi