KWA NINI NENO LA SIKU?
1.Neno
la Mungu linatoa dira ya maisha ya mtu:Ili
maisha yako yawe na uelekeo sahihi hunabudi kulijua Neno la Mungu ili
likuongoze katika hatua zako za kila siku. “Neno lako ni taa ya
miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.”ZABURI 119:105
2.Neno
la Mungu linafundisha na kuonya :Maarifa yote
ambayo mwanadamu anayaitaji katika maisha yake ya kila siku yanapatikana katika
Neno la Mungu. Pia Neno la Mungu lionya na kuelekeza kwa namna gani mwanadamu
anapaswa kuishi. “Kila andiko, lenye pumzi
ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa
kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;”2 TIMOTHEO 3:16
3.Neno
la Mungu ni kinga dhidi ya dhambi:Mtu anayelijua
Neno la Mungu na kuliishi sawa sawa na jinsi linavyomwelekeza dhambi hazipati nafasi ndani ya moyo wake.Ni
tofauti na mtu ambaye amekariri maandiko pasipo kulijua hayo maandiko yanampasa
kufanya nini? “Moyoni mwangu nimeliweka
neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.”ZABURI 119:11
4.Mungu
anasema na watu wake kupitia Neno lake:
Unaweza kumsikia Mungu kupitia njia mbalimbali.
Comments
Post a Comment