Skip to main content

MAMBO 5 KUKUSAIDIA KUFIKIA MALENGO YAKO

MAMBO 5 YANAYOWEZA KUKUSAIDIA KUTIMIZA MALENGO YAKO KWA WAKATI.
1.         Anza mapema utekelezaji wa malengo yako,”Wahenga wanasema mambo mazuri hayahitaji haraka” lakini napenda kukushauri kwamba unapopata wazo zuri katika malengo yako usisubiri sana, ukikaa na wazo muda mrefu sana bila kulifanyia kazi utasahangaa uzito wa wazo lako unapungua siku hadi siku.
"wazo/lengo siyo lako mpaka uanze kulifanyia kazi ndiyo litakuwa lako" waweza kuwa na malengo mazuri na makubwa tena makubwa ya kuleta mapinduzi makubwa, lakini kama hujaanza kuyawekea utekelezaji mapemayatabaki kuwa mawazo. jitahidi kuanza mapema kutekeleza juu ya malengo yako.
2.         Usitumie muda mwingi kuwaza na kusimulia watu juu ya Malengo, usimushirikishe kila mtu katika Malengo yako Bali angalia watu wanaofanya kile ulicholenga kukifanya, kwa mfano kama lengo lako ni kufungua biashara, angalia watu wanaofanya biashara inayofanana jaribu kuwashirikisha upate undani wa biashara yenyewe'
       Dada Amina Wa Sanga anasema "Usimuamini kila mtu, usimuweke karibu kila mtu. Kuna vitu kaa navyo mwenyewe mpaka vitokee, wengine wangeshakua wamefanya vitu vikubwa, wengine wangekua wameandika vitabu vingi, hawachukui hatua kwasababu wanataka kueleweka. Usilazimishe watu wakuelewe, sio lazima. WE PAMBANA, You're the captain of your own ship.
3.        Usiogope kufanya kazi Kwa bidii kutumiza lengo lako yaani usijionea huruma, unapoweka Malengo yako usijionee huruma, piga kazi usiku na mchana mpaka uone njia ya kukufanikisha kufikia malengo yako.
4.        Ongeza ufahamu wako (maarifa) kuhusu Malengo yako, Jitahidi kutafuta Maarifa ya nyongeza kuhusu Malengo yako, hapa soma vitabu na taarifa mbalimbali zinazohusu malengo yako. Tafuta taarifa sahihi kuhusu wazo lako, hakikisha unakuwa mwalimu wa malengo yako kwa utajiri wa taarifa na maarifa uliyonayo.

5.        Weka usimamizi mzuri wa Malengo yako na ujenga nidhamu ya pesa na matumizi ya muda wako. Ukitaka kufanya vizuri katika kuelekea malengo yako, jitahidi kuweka usisimamizu mzuri, pangilia vizuri ratiba zako na ujenge nidhamu ya kutosha katika kuzifikia ndoto zako.
@alfredmwahalende
@yopocode
@nanenanefestival2018
https://yopocodetanzania.blogspot.comhttps://yopocodetanzania.blogspot.com

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi