Skip to main content

ZAO LA MUHOGO

ZAO LA MUHOGO
UTANGULIZI
Zao la mihogo ni muhimu  . Hata hivyo wakulima wengi bado wanatumia mbegu za asili ambazo hutoa mavuno kidogo. Jitihada zinafanywa za kusisitiza matumizi ya aina ya kisasa hususan Kiroba ambayo inaukinzani na ugonjwa wa mihogo uitwao batobato. Faida ya zao hili ni kwamba hustahmili ukame, mizizi, miti na majani hutumika kwa chakula mbegu na mboga, pia huweza kukaa ardhini kwa muda mrefu bila kuharibika
 AINA ZA MIHOGO
Zipo aina mbali mbali za mihogo za asili lakini kwa sasa inashauriwa kutumia aina za kisasa ambazo ni: Kiroba na Msitu Zanzibari kwa sababu hukomaa haraka na kutoa mazao mengi. Pia Kiroba inaukinzani na ugonjwa wa batobato wa mihogo.
UTAYARISHAJI WA SHAMBA
Shamba la mihogo ni vema litayarishwe mapema kwa kukata miti, vichaka kisha tifua vizuri kiasi ya sm 15 hadi 30. Aidha shamba linaweza kutayarishwa kwa kutumia matuta.
UPANDAJI NA NAFASI ZA KUPANDIA
Mihogo hupandwa pingili zilizochaguliwa kutoka katika mimea iliyokomaa vizuri na isiyo na ugonjwa. Pingili hukatwa kwa kisu kwa urefu wa sm 30 hadi 45 tayari kwa kupelekwa shamba
ili zipandwe. Mihogo hupandwa kwa nafasi ya sm 120x90 kwenye shamba la sesa na sm 150x75 kwenye shamba la matuta.
Sio muhimu kutumia mbolea za kupandia za viwandani isipokuwa iwapo shamba halina rutuba inashauriwa kutuima samadi kiasi cha tani 4 hadi 5 kwa eka.
PALIZI
Palizi huanza baada ya wiki mbili toka kupandwa na jembe la mkono hutumika na kurudia mara kwa mara mpaka mihogo inapokomaa. Hakuna haja ya kupunguza miche kwa sababu hupndwa pingili moja kwa shina.
MBOLEA ZA KUKUZIA
Mbolea za viwandani sio muhimu kwa zao la muhogo.
DHIBITI YA WADUDU
Wadudu wanaothiri mihogo ni mchwa, vidugamba na inashauriwa kutumia dawa aina ya Karate au Decis kiasi cha cc125 kwa lita 20 za maji.
MAGONJWA
Mihogo huathiriwa zaidi na ugonjwa wa bato bato kali kwenye majani pamoja na ule wa kuoza mizizi. Magonjwa haya hukingwa kwa kuanda mbegu ambazo hazina ugonjwa au kutumia aina ya mihogo yenye ukinzani ambayo ni Kiroba. Pia inshauriwa kutumia kanuni za kilimo bora ilikupunguza athari ya magonjwa haya.
UKOMAAJI NA UVUNAJI
Mihogo hukomaa baada ya miezi 12 had 18 kutegemea na aina ya mihogo, hali ya hewa pamoja na utunzaji. Mihogo iliyokomaa ivunwe kwa kungoa mashina na eka moja iliyotunzwa vizuri hutoa tani 4
hadi 10.
HIFADHI NA UUZAJI

Mihogo iliyovunwa humenywa na kukaushwa juan ili ikauke vizuri. Mihogo iliyokaushwa husagwa unga na kuuzwa au huhifadhiwa kama makopa kwa matumizi ya baadae

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi