Skip to main content

MAMBO YA KUFANYA ILI MUDA WAKO UKULETEE MAFANIKIO

MAMBO YA KUFANYA ILI MUDA UKULETEE MAFANIKIO.
Mwalimu Subira Mlaga
1. Chagua kitu cha kufanya:Haijarishi una mipango mingi kiasi gani.Toa vipaumbele katika mipango yako uliyojipangia.Pasipo kuwa na vipaumbele unaweza tamani kufanya kila kitu ndani ya muda mmoja.Unapoweka vipaumbele vinakusaidia kujua kitu gani uanze nacho na kitu gani kimalizie. Na kwa muda gani uwe umekamilisha na kuanza jambo lingine.Unapochagua ufanye nini na nini usifanye itakusaidia kukomboa muda.
2. Tenda jambo sahihi kwa muda sahihi:Kila jambo lina muda wake.Ili ufanikiwe zaidi ni muhimu kufanya kila jambo kwa muda  sahihi.Mfano wewe unauza duka,muda wa kuwahudumia wateja wewe upo busy whatsup,instergram,fb unachati,mara kidogo unasuka nywele dukani ukweli ni kwamba unawapa wakati mgumu wateja wako hata kama hawatakuambia.Sasa wateja wakikuama utaanza lalamika,kuwa duka la jirani mchawi kahamisha wateja wako.Kumbe mchawi ni wewe mwenyewe umeshindwa kufanya jambo sahihi kwa muda sahihi.Ukiwa dukani mteja anategemea akukute upo tayari kumuhudumia kwa muda sahihi,sasa kama wewe hautajali muda wateja watakuhama.Na watakwenda huko ambapo muda wao utathaminiwa.Kama haujali muda,mafanikio utaishia kuyasikia kwa jirani.
3. Tenga muda wa kutosha katika jambo unalotaka kulifanya:Kuna wakati umefanya uchaguzi sahihi wa nini kifanyike,ukafanya jambo hilo kwa usahihi lakini umeshindwa kufanikiwa kwa sababu haukutenga muda wa kutosha.Mafanikio ya kudumu yanahitaji muda wa kutosha.Na hilo jambo lako lipe muda wa kutosha,usikurupuke wala usiingilie mipango mingine kabla ya kukamilisha mipango ya awali.Mfano  umeanza kufuga kuku wa mayai mtaji wa kutosha unao mpaka chenji ina baki.Lakini ufugaji huo usipoupa muda wa kutosha hautaona mafanikio yoyote.Unapokuwa na muda wa kutosha inakusaidia kujua vyema lile jambo unalotaka kulifanya,hautalifanya kwa kubahatisha bali utafanya kwa uhakika.Hata changamoto zijapo utakuwa ngangari na tayari kusonga mbele.Kila jambo ulifanyalo lipe muda wa kutosha.
4. Yawezekeza muda wako kwenye ndoto zako:Watu wengi leo hawajafanikiwa na uenda wasifanikiwe kabisa kwa sababu wamewekeza muda wao kwenye ndoto za wengine na wamesahau kuziishi,ndoto zao.Mfano wewe ni mwalimu kama mimi una ndoto ya kuwa na chuo chako,au shule yako.Unapaswa kuweka mipango madhubuti ya kufikia ndoto yako.Ni kweli umeajiriwa lakini usiterekeze ndoto zako.Tenga muda kwaajili ya ndoto zako
5. Kaa mahali sahihi:
Ukifanya jambo sahihi mahali pasipo sahihi si rahisi kufanikiwa.Ukiwa mahali sahihi kwa muda usio sahihi hautafanikiwa.Haijalishi umejitoa kwa kiasi gani.Hata kama wewe ni time keeper kama haupo eneo sahihi utaendelea kupoteza muda.Tafuta eneo sahihi la wewe kuwepo.Mfano unafanya kazi kama mwalimu,kumbe wewe ulipaswa kuwa mkandarasi.Unapoendeleakuwa mwalimu hautafanikiwa kwa sababu siyo eneo lako.Unapokuwa eneo sahihi ni rahisi kufanikiwa.Tafuta na ulijue eneo la mafanikio yako lipo wapi?Siku utakapolijua hautapishana tena na mafanikio yako.
6. Jitahidi kubalance muda wako:Natambua umuhimu wa kuwajibika,pamoja na kuwajibika huko jitahidi kupangalia mambo yako vizuri na muda wa kutosha wa kuyatekeleza.Ukishajua vipaumbele vyako ni vipi jitahidi kuvipa muda wa kutosha.Mfano wewe ni mwanamke na una familia,mfanyakazi,mjasiriamali,na mengine unayafanya ili ufanikiwe unapaswa kubance muda wako.Muda wa familia usiingiliwe na biashara,muda wa kazi uwe muda wa kazi.Ukifanya hivyo utafanikiwa kwa sababu kila jambo umelipa muda wake.




Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi