Skip to main content

NENO LA MWAKA

NENO LA MWAKA
² "Basi imani ni hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana."EBRANIA 11:1.
² Unapokuwa na imani ina maana unao uhakika wa mambo yote unayoyatarajia yatoke katika maisha yako.
² Imani ina sababisha mambo kutokea katika maisha yako, ukiwa na imani haba utapokea haba katika matarajio yako.
² Ukiondoa imani ndani ya moyo wako utakaribisha hofu, mashaka na wasiwasi ambayo uvuruga mipango ya Mungu kwako.Watu wengi wameshindwa kufanikiwa katika mipango yao kwa sababu ya kukosa imani.
² Kukosa imani kunamfanya mtu akate tamaa kuyaendea mafaniko yake.
² Mtu asiye na IMANI katika moyo wake huendeshwa na mitazamo na kilele za watu wanamzunguka, hujiuliza maswali ya kushindwa na kukatisha tamaa kabla hajajaribu kufanya jambo.
² Endelea kumwamini Mungu juu ya ahadi zake maishaini mwako nae atafanya mambo makubwa na utamshangaa mungu anavyoonekana katika mipango yake kwake.
² Nataka niseme na wewe unayemwamini MUNGU kuwa ndiyo kimbilio lako ya kwamba huna sababu ya kuogopa kitu kwa kuwa ahadi ya Mungu kwako ni kukufanikisha kwa kila jambo.
² UKIWA NA IMANI UNA UHAKIKA WA KILA JAMBO LA BAADAE.


Comments