Skip to main content

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania
Na Alfred Mwahalende
Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo:
1.    Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa.
2.    Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi.
JE, UJANA NI NINI?
3.    Ujana ni hatua ambayo mtu anapitia baada ya utoto.
4.    Ujana ni hali ya kuwa na tabia za umri wa ujana ambao ni miaka 18-35.
5.    Ujana ni kipindi cha makuzi ya mtu kabla ya utu uzima na hatimaye uzee.
6.    Ujana ni kipindi kati ya miaka 18-35 hivi ambapo mtu anakuwa amepevuka na ukomavu wa kiakili na kimwili.
NIKUKUMBESHE MAMBO KUMI NA MBILI (12) MUHIMU UNAYOTAKIWA KUYAFANYA KATIKA KIPINDI HIKI CHA UJANA WAKO;
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unajijenga kielimu, imarisha misingi kwenye taaluma mbalimbali yaani elimu ya msingi ya darasani na elimu ya stadi za maisha ya mtaani. Jijengee Maarifa makubwa yatakayokusaidia kuhamisha milima yaani changamoto. Pia katika elimu usisahau elimu ya dini, elimu ya afya, biashara, ujasiriamali na mahusiano.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unapata ardhi au kiwanja chako na uanze kuweka malengo ya kujenga.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 wekeza kwenye chochote unachohisi au unachoona kinaweza kukuingizia kipato chako, usiogope kuwekeza kwenye fursa ndogo ndogo zinazoweza kukuingizia kipato.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unaingia kwenye mahusiano ya kweli na ndoa. Unapofikia ujana hakikisha unajijengea mahusiano mazuri, unitumie silaha ya ujana kujiingiza katika mahusiano na kila inayemuona mbele yako. 
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unakwepa kujiingiza kwenye starehe zisizokuwa za lazima, achana na tabia za ulevi, matumizi mabaya ya muda na pesa, kumbuka wakati wa ujana ni wakati wa kukusanya utakachokula uzeeni.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unafungua akaunti ya pesa ili uweze kuanza kuweka akiba kwa matumizi ya baadaye.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unajenga uaminifu kwa kila mtu yaani uaminifu katika ahadi na matendo yako.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unakuwa na marafiki wenye tija, pia marafiki wanakujenga kiakili na kukusaidia kutimiza kusudi lako, achana na marafiki wanafiki, wafitini na wenye wivu wa kijinga. Pia angalia marafiki wanaokutia moyo na kukukosoa pale unapokosea.
https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v8/fe/1/16/2733.png
 katika kipindi hiki cha ujana hakikisha unaanza kufanya mambo yako kwa malengo. Usifanya mambo bora yaenda, Fanya mipango kwa utuluvi mkubwa usikurupuke, weka mikakati makini inayoweza kukutoa katika maisha yako. 




Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana