Skip to main content

KULIJUA KUSUDI

NA MWANDISHI, SUBIRA MLAGA

KULIJUA KUSUDI.
Hakuja jambo linalofanyika kwa bahati mbaya, kila jambo linalofanyika kuna sababu inayosababisha lifanyike kwa jinsi unavyoliona.

KUSUDI:Ni sababu inayofanya mtu,au kitu kuwepo pale kilipo. Mfano kisu unapokuwa nacho kinalitumikia kusudi la kutengenezwa kwake.Kisu utakitumia kurahisisha shughuli zako mbalimbali.Pale kisu kinapokupa urahisi wa kazi yako hapo kinatimiza kusudi la kutengezwa kwake.
💎Binadamu Mungu alipomuumba alimwekea kusudi ndani yake.Haijarishi unajua au haujui kusudi la kuumba kwako aina maana kuwa Mungu alikuumba bila ya kusudi.Katika kitabu cha mwanzo wakati Mungu akimuumba mwanadamu aliweka sababu kwa nini anamuumba."Mungu akasema,Na tumfanye mtu kwa mfano wetu ,kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini na ndege wa angani,na wanyama,na nchi yote pia,na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi."MWANZO 1:26. Hapa inaonekana sababu ya kuumbwa mwanadamu kuwa atawale vitu vyote Mungu alivyo viumba.Jiulize swali na mimi pale ulipo wewe ni mtawala au mtawaliwa??Kama unatawaliwa huo siyo mpango wa Mungu utawaliwe bali utawale.

AINA ZA KUSUDI.

kuna aina kuu 2 za kusudi katika maisha ya mwanadamu.

1. KUSUDI KUU/GENERAL PURPOSE.
Mungu alipokuumba alikusudia uwe mtawala wa vile alivyoviumba.Mungu anafurahi akiona una mamlaka .Kuwa na mamlaka hakuishi tu Kuwa na cheo kazi hata kuwa na mamlaka na kazi za shetani,shetani hasikutawale kwa sababu ukiibwa utawale. "Lakini nasema ya kuwa mrithi,wakati wote awapo mtoto,hana tofauti na mtumwa,angawa ni bwana wa yote"GALATIA 4:1.Hata na wewe kama haujui haki zako utaendelea kutawaliwa kila mahali.

2. KUSUDI MAALUMU/SPECIFIC PURPOSE.
Kuna kusudi maalum kwa kila mtu mahali popote alipo.Makusudi haya yametofautiana kutoka mtu moja hadi mwingine:

I)Kusudi la wito:Wewe mtumishi unayemtumikia Mungu katika huduma yoyote je unajua sababu ya wewe kuwa mbele za Mungu??Mungu hajakuita tuu ana sababu na wewe katika ualimu wako,uchungaji wako,uimbaji wako n.k.Kusudi la Mungu kukuita katika wito uliona ni ili umuwakilishe yeye na siyo kujionyesha wewe."Mtu na atuhesabu hivi,kuwa tu watumishi wa Kristo,na mawakili wa siri za Mungu". 1KORINTO 4:1

II)Kusudi katika ndoa/familia:Katika familia uliyopo Mungu ana kusudi na wewe,na Katika ndoa uliyofunga Mungu anakusudi nayo.Yamkini kutokana na mapito na taabu ukaanza kumlamu Mungu Kwann mume Wang hivi,watoto  n.k pamoja na hayo Mungu bado anakusudi anakusudiapo weweo.Ukilijua kusudi la wewe kuwa katika familia  hiyo hautapata shida. hautapataII)Kwanasumbua

FAIDA ZA KULIJUA KUSUDI.
1. Utafanya bidii ufikie ndoto/Hatima yako.Unapolijua kusudi la kuubwa kwako hiyo ni dira inayoonyesha uelekeo wa ukuu wako.

2. kilijua kusudi hautaambatana na kila mtu. Unapolijua kusudi ni sawa na mama mjamzito ambaye anajichunga baadhi ya mambo asifanye ili mtoto aliyembeba awe salama.Na wewe unapolijua kusudi hautaambatana na kila mtu ili ufike kwenye kiilele chako.Kuna watu ukiambatana nao wanaua na kupoteza muda wako.Angalia sana nani unaambatana nae.
3. Ukilijua kusudi la kuumbwa kwako utafurahia maisha.Furaha ya kweli katika maisha ya mtu inapatikana kwenye kusudi.Ili ufirahie maisha haina haja ya kuumiza kichwa muombe Mungu akupe kulijua kusudi la kuumbwa kwako.Usimtegemee mtu akufurahishe,tumikia kusudi la kuubwa kwako ufurahie maisha.

4. Hautafanya kila kitu.Ukilijua kusudi litakuongoza ufanye nini na utajizuia usifanye kile kilicho kinyume cha kusudi lako.

5. Kusudi litakutofautisha na wengine.Kuna watu ni ngumu  kuwatofautisha kwa sababu wana copy na kupaste vya watu.Watu  hawajawahi kuishi maisha yao.Hata bidhaa utofautiana kutokana na matumizi.Tafuta kujua kusudi.



Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi