Skip to main content

KUWA MSHUMAA WENYE MAANA NA FAIDA KWA WENGINE

Image result for HELPING OTHERS AS A CANDLE LIGHTING OTHER CANDLE PICTURES


Zig Ziglar aliwahi kusema kwamba Ukitaka kufanikiwa saidia wengine kufanikiwa na wewe utafanikiwa na mimi nakwambia kwamba Ukitaka kuangaza dunia nzima kuwa mshuma ambao unawasha mishumaa mingine sio kuizima ya wengine.Ukiwa na nafsi ya kutaka mshuma wako tu kuangaza dunia nzima hautafika sehemu yoyote itazima tu na wala hautakuwa na nguvu ya kuangaza mbali.Watu hawatasema kwamba huyu mtu alishawahi kuwasha mshumaa wake hata siku moja.
Naomba nikueleweshe kitu kuhusu huu mshumaa, mishumaa nimeivisha taswira ya MAARIFA YAKO, NDUGU, JAMAA, MARAFIKI ZAKO ambao wanakuzunguka.

1. Mshumaa Ni watoto wako Kama hutaweza kuwapa maarifa ya dunia ambayo umeweza kuyaona na kuyatatua hata siku ukiwa haupo hawatatambua uwepo wako. Ila Kama utaweza kukaa chini na kuzungumza nao pindi usipokiwepo watajua kuwa baba au mama walitusaidia kwelii na watu watasema kwelii wale watoto ni wa flani. Watoto wanachohitaji ni zawadi ambayo unayo ndani yako kama ni maarifa basi hauna budi kuwapa pia. 
Unapotumia mshumaa wako kuwasha ya wengine unaongeza nguvu ya dunia kuondokana na giza nene, na unazidi kuonesha kwamba kumbe peke yako hauwezi kuangaza dunia nzima bila kusaidia wengine kuwasha yao, mshumaa wako ukiwa chanzo cha mishumaa mingine kuwaka utatengeneza dhana ya kwamba bila kusaidia mwingine mshumaa wako sio kitu. Unaposaidia wengine unasaidia hata ambao huwajui kusaidia wasaidie wale ambao huwajui mishumaa yako kuwasha. Kumbuka kwamba hata ikizima bado ya wengine itasaidia kuwasha ya wenzao.

2. Mishumaa hii ni rafiki zako jinsi unavowasaidia kuwapa maarifa tofauti na kuweza kuwasaidia kimawazo. Unaposaidia marafiki zako ni sawa na kujisaidia mwenyewe ila usiposaidia marafiki haujajisaidia mwenyewe. Vipi mshumaa wako ukizima nani atauwasha ukiwa katika safari yako ya mafanikio wakati unaoongozana nao hukutaka kuwasha hata wa mmojawapo?? Kuwa makini.  

Mpenzi msomaji wa makala hii katika mtandao wa YOPOCODE TANZANIA napenda kukwambia kwamba ukiweka MSHUMAA wako katika kilele utaangaza na utaleta maana yake ya kuangaza na kuweka kileleni maana taifa zima litanufaika, hapa namaanisha tuzidi kujinoa na kitu kionekane na kizidi kuleta manufaa katika jamii zetu.Ila unapoficha MSHUMAA wako chini ya uvungu wa kitanda haitakuwa na maana ya kuuwasha. hapa namaanisha kwamba unapoamua kufanya jambo la kusaidia jamii yako usilifiche kwa kuogopa watu, ila litoe limulike na wengine na kuwasha mishumaa ya wengine hapo utakuwa umeweka tafsiri maalumu ya mshumaa wako. 

Kwa wewe ambae unahitaji kupata mwongozo katika shughuli zako za biashara maendeleo binafsi na mahusiano napenda kukukaribisha katika program ya AKILI YA USHINDI kupata maelezo ya kuwa mwanachana bonyeza https://akiliyaushindi.com/ nenda katika menu sehemu KUHUSU AKILI YA USHINDI.

Ulikuwa nami;

Coach Lazaro Samwel
0753616584/0653386586
Email; lazarosamweli41@gmail.com

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi