Skip to main content

HAKUNA LISILOWEZEKANA KWA MUNGU.

HAKUNA LISILOWEZEKANA KWA MUNGU.
MWALIMU SUBIRA MLAGA
💦Kuna mambo kwa akili za kinadamu yanashindikana, akili ya kibinadamu inafika mwisho. Pale akili yako inapofika mwisho hapo ndio mwanzo wa akili za Mungu. "Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema BWANA. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu."ISAYA 55:8_9.

💎Yamkini kuna hali,majaribu na mapito mbalimbali unapitia sasa,watu wako wa karibu wamekukatisha tamaa kuwa hilo jaribu/pito/shida yako haiwezekani tena.Labda ni dokta kutokana na vipimo akakuvunja moyo kuwa hutapona tena,hautazaa tena na n.k.
Leo nakumbia habari za Mungu mwenye uweza wa mambo yote hakuna jambo lolote la kumshinda yeye.Ukimwamini sasa atafanya yasiyowezekana katika macho ya wanadamu kuwezekana  na kuwashangaza waliokubeza.
Haikuwa rahisi kwa ajuza Sara kuamini katika umri wa miaka tisini matiti yake yangenyonyesha mtoto wa kumza.
Lakini tunaona Mungu akimtokea Sara na kumpa mtoto katika umri mkubwa ambapo wanasayansi akili zao zinagoma katika umri mkubwa vile mwanamke kuzaa mtoto.
"Ndipo Ibrahim akaanguka kifudifudi akacheka,akasema moyoni,
Je!Mtu wa umri wa miaka mia,kwake atazaliwa mtoto?Naye Sara mwenye umri wa miaka tisini atazaa?"MWANZO 17:17,"BWANA akamwambia Ibrahimu,Mbona Sara amecheka akisema,Mimi kweli nitazaa mwana,nami ni mzee?Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA?..."MWANZO 18:13_14.
Hakika hakuna la kumshinda Bwana.Hata kama Ibrahimu na Sara walishajikatia tamaa tunaona kwa majira yaliyokubarika Isaka anazaliwa.

💎Unaona mambo magumu hayawezekani kwa sababu haujampa Mungu nafasi ya kudhihirisha uweza wake katika maisha yako.
"Tazama mimibni BWANA,Mungu wa wote wenye mwili;je !Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?YEREMIA 32:27.Mungu anatushanga kuwa hatumtegemei na kumwamimi kwa 💯🐥%kuwa yeye anaweza.Anza leo kuwamwani Mungu yeye anaweza na hakuna la kumshinda.

💎Katika mapango na malengo yako uliyonayo nakusihi usiwaze na hofu kuwa itakuwaje?Ni kweli siku zimeenda na miezi imesogea labda haujapata kazi,mke,mume n.k. Namutia moyo hata hayo usipoyaona kwako haina maana kuwa Mungu hawezi tena kukutendea kwa sababu yeye ni Mungu wa wote wenye mwili hivyo na la kwako analiweza pia."Kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu"LUKA 1:37
KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA.


Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi