Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2018

KUHUSU KITABU CHA DIRA YA KIJANA TANZANIA

KUHUSU KITABU CHA DIRA YA KIJANA TANZANIA Ni kitabu pekee kilichobeba elimu stahiki ya stadi za maisha kwa vijana na chenye ubora wa hali ya juu kinachochambua na kutoa dira ya safari ya maisha ya kijana na miongozo inayotoa ramani ya kumsaidia kijana kujisimamia  mwenyewe na kujiajiri  kwa kutumia fursa mbalimbali za ujasiriamali zilizopo kama vile uwekezaji katika sekta ya  viwanda, kilimo biashara, ufugaji wa kisasa, madini, biashara ndogo ndogo, za kati na kubwa zilizopo katika jamii na kuweza kuendesha shughuli za uzalishaji mali na maisha yao bila kutegemea usimamizi kutoka kwa mtu mwingine ( kuajiriwa). K itabu hiki ni chachu ya mabadiliko chanya kwa vijana na kinatoa hamasa na ku wachochea vijana kushiriki katika harakati za kuleta maendeleo katika jamii zao na kukubali mabadiliko ya kisera na kuacha kukaa vijiweni kulia na kulalamika juu ya hali ngumu ya kimaisha (vyuma vimekaza) na ukosefu wa ajira katika sekta za serikali na mashirika binafsi na badala yake wa shiriki