Skip to main content

KANUNI ZA KILIMO BORA

KANUNI ZA  KILIMO BORA 
NA MWANDISHI WETU
Misingi na kanuni za kilimo bora.
Neno Msingi lina maana ya mwanzo wa kufanya shughuli yeyote inayokusudiwa ili kuweza kufikia malengo. kwa hiyo katika kilimo ipo misingi muhimu ifuatayo:
Kuwa na mipango thabiti inayotekelezeka kabla ya kuanza kufanya kazi yeyote ya maendeleo ni vyema, kuweka mpango kazi ili iwe dira wakati wa utekelezaji. Hivyo wakulima wanatakiwa waweke malengo yao ya kilimo kwa kuangalia Usalama wa chakula na kipato
Mipango bora.
Ni mipango ambayo inamsaidia mkulima kupata chakula cha kutosha na fedha ili kuondokana na umaskini. Mipango inatakiwa iwe shirikishi kwa kuona kuwa wakulima wana shiriki katika kupanga, kutekeleza,  kufuatilia pamoja na kutathmini.
Kuchagua eneo linalofaa kwa kilimo.
Kwa kuwa kilimo ni kazi ya kisayansi, eneo linalofaa kwa kilimo liwe na rutuba, mteremko wa wastani, liwe sehemu inayopitika ili kurahisisha usafirishaji wa mazao na pembejeo wakati wa uzalishaji.
Uwekaji na utunzaji wa kumbukumbu.
Ni muhimu mkulima kujiwekea kumbukumbu za uzalishaji, mapato na faida ili kupima mafanikio ya kazi yake.
Matumizi ya kanuni za kilimo bora.
Neno kanuni lina maana ya utaratibu wa kisanyansi uliofanyiwa majaribio kwa muda mrefu na ambao umekubalika utumike wakati wa uzalishaji wa mazao.
Kanuni za kilimo bora
*  Kutayarisha shamba mapema Kwa kutifua.
*  Kupanda mbegu bora kwa nafasi inayostahili.
*  Kupunguzia miche na kubakiza inayoshauriwa
*  Palilia mapema-si zaidi ya wiki mbili baada ya kuota mazao..Plazi ziwe mbili au zaidi.
*  Weka mbolea ya kukuzia mara baada ya palizi.
*  Weka dawa ya kuua wadudu wa mimea.
*  Linda mazao yako na Wanyama waharibifu Vuna mazao yako baada ya kukomaa vizuri.
*  Sindika mazao yako na kuyaweka kwenye mifuko inayoingiza hewa baada ya kuweka dawa.

*  Hifadhi mazao mahali pazuri pasipo vuja au kufikiwa na wanyama waharibifu.( Panya)

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi