Skip to main content

WANAHITAJIKA MAWAKALA

WANAHITAJIKA MAWAKALA

TanzaRice International inauza mchele mtamu wa Mbeya, uliochambuliwa, kusafishwa na kisha kufungwa vizuri katika mifuko standard ya kilo tano (5) inayouzwa kwa namna ya kibunifu inayowezesha walaji na wasambazaji kunufaika kifedha.

Kampuni inatafuta mawakala 60 wa bidhaa zake katika viunga mbalimbali vya jiji la Dar es Salaam ili kusogeza Huduma karibu na wateja kote jijini.

Sifa za Mwombaji
1. Awe na umri usiopungua miaka 18
2. Awe mtaji wa sh. 200,000/= na kuendelea
3. Awe na biashara au anataka kufanya biashara
4. Awe na simu/kompyuta yenye uwezo wa internet
5. Awe mwaminifu na mchapakazi.

Wakala wa TanzaRice anapata faida ya sh. 1,000/= katika kila mfuko anaomuuzia mwanachama wetu na sh. 3,000/= katika kila mfuko anaomuuzia mteja wa kawaida. Pia kampuni inamlipa sh. 2,000/= kwa kumsajili mwanachama mlaji mpya. Zaidi ya yote,  wakala pia anapata kamisheni na bonus Kama wanachama wengine inayotokana na ulaji wa mchele wa TanzaRice.

Iwapo una sifa zilizotajwa hapo juu isipokuwa tu mtaji ulionao ndio pungufu ya 200,000/= unaweza pia kujaza fomu au kuwasiliana na kampuni.

Mafunzo ya namna ya kupata masoko, namna ya kusajili wanachama walaji na namna ya kuwahudumia wateja yatatolewa bure.

Kuomba kuwa wakala, jaza fomu hii hapa chini 👇👇

https://goo.gl/forms/hu9Zemksj1AsJENq2

Kwa maelezo zaidi unaweza kupiga simu/whatsapp namba 0753506958

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi