Skip to main content

NJIA NGUMU; Kurasa 12 kitabu cha kwanza cha mwaka mpya HATUA kubwa 2018/19

NJIA NGUMU; Kurasa 12 kitabu cha kwanza cha mwaka mpya HATUA kubwa 2018/19

Kitabu; WAR of SELF, The 7 Weapons of Self Mastery by Ramman Sheehan Turner ( Vita ya Binafsi, Silaha 7 za Ubobezi binafsi ) 60 ~ 72

SILAHA ya 3; Ona Ukweli katika udanganyifu na wewe ni sehemu ya Ulimwengu mzima ona mahusiano ya uwepo wako na watu na mazingira asilia yanayokuzunguka.

HATUA ya KUCHUKUA; Ona uhalisia ulivyo na kila mara jua u sehemu ya ulimwengu na acha kujidanganya mwenyewe.

Rafiki ukweli ni silaha yetu ya tatu ambayo itaondosha ugomvi ndani yako na kukuweka huru katika maisha yako. Pale unapoondoa ukweli basi unaangukia kujidanganya na ukijidanganya unajiweka katika kifungo. Je uko tayari kuishi maisha yako katika kifungo ikiwa waweza kuwa huru kwa kusema kweli au kujua kweli?. au ukweli wa mambo. Basi moja ya jambo ambalo watu wanajidanganya ni kujiona wao si sehemu katika ulimwengu, wanaona kuchukua au kutochukua hatua kwao hakuna athari katika Dunia. Si kweli kuwa athari yako haipo ipo ikiwa utaona kuwa u sehemu katika ulimwengu tunaoishi.

Dunia na mazingira yake yako katika mahusiano makubwa na mahusiano haya yanashuka hadi ngazi ya uwepo wa viumbe wake namna kuishi kwao kulivyo na mahusiano yanayoweza kutoa athari toka chini hadi juu kabisa ngazi ya mahusiano ya watu wa mataifa mbalimbali. Uwepo wa teknolojia hasa eneo la mawasiliano ndio umefanya eneo moja katika Dunia kuweza kufanya athari ionekane eneo lingine pia na hata ulimwengu mzima ( ona ilivyo Simu janja ujifunze kitu ) . Mfano katika habari moja ya eneo lingine yaweza kuathiri maeneo mengi ya Dunia sababu tu sehemu sasa ya umoja katika Dunia.

Je kitu gani huwa unakiona katika kila jambo unalolisikia katika taswira uonayo na jinsi uhalisia utakavyokuwa ukiingia kufanya hicho kitu au kikikupata ?. Kama unapuuza uhalisia wa mambo utakavyoenda kuwa basi utajitengenezea ugumu mwenyewe. Ili kupata amani na furaha katika kuishi kwako basi ni muhimu sana kuona mambo kama yalivyo katika maisha yako. Ona mambo kama yanavyotakwa kuonwa na uone jinsi ulivyo nawe ni sehemu ya jamii katika ulimwengu tunaoishi. Hatua hii ni silaha kwako ya kuondoa ukinzani ndani yako kila siku za kuishi kwako. 

Endelea kufuatilia kurasa hizi 12 kila siku kuna hatua utavuka ya HATUA KUBWA kwa maisha yako ya kila siku.

Mchambuzi mwanafunzi eneo la Uhalisia wa Maisha
Mwanafunzi wa Kilingala 
Mchambuzi wa vitabu
Mwandishi wa vitabu
Mfanyabiashara wa maarifa/taarifa ( INFOPRENEUR )
Malenga wa Ubena
© Raymond Nusura Mgeni 2018
+255 676 559 211 au +255 766 461 571
raymondpoet@yahoo.com

SAFARI ya V 450, 2023 Hatua moja huanzisha safari.

Mafanikio ni kujitoa na maisha ki uhalisia ni mchezo wa akili kubwa. Nimejitoa kulipia gharama kufikia HATUA KUBWA.

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi