Skip to main content

VIKUNDI VYA VIJANA VYA UJASIRIAMALI


NAMNA YA KUENDESHA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI NA BIASHARA

Name; FILBERT NYONI
Phone no; 0656447888
       email; nyonifilbert30@gmail.com

Vijana wenzangu popote mlipo Tanzania na duniani kote,poleni kwa mahangaiko ya kuendelea kutafuta ugali kwani hata katika maandiko ya vitabu vya dini imeandikwa asiyefanya kazi na asile,na mwanaume atatafuta kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu,hii yote ni kudhilisha kuwa ni lazima kila mtu afanye kazi kulingana na kipawa alichojaaaliwa na mwenyezi mungu muumba wa mbingu na vyote vilivyopo katika uso wa duniani.
Najua kila kijana ananamna anavyotafuta RIDHIKI ili mradi tu inakua halali, wapo wanaofanya kazi mmoja mmoja,wapo walioajiriwa serikalina, taasisi za serikali, taasisi na mashirika binafsi, lakini wapo ambao wameamua kujiajiri wenyewe katika shughuli mbalimbali za kijasiariamali, wapo wakulima, wafanyabiashara, mmoja na hata walioamua kuunda vikundi ili kuona namna gani nguvu ya pamoja inaweza kuwafikisha pale wanapotaka kufika, yote kwa yote mkono unaingia kinywani. Leo ni fursa kwa wale ambao wameamua kuwa katika vikundi mbalimbali vya ujasiriamali na biashara, kuweka na kukopa n.k kwani watajifunza mengi kupitia makala hii.
Maana ya neno kikudi…….
Kikundi ni mkusanyiko wa watu kadhaa wenye rika tofauti au linalofanana, jinsia moja au tofauti ambao walioamua kufanya shughuli za kujiingizia kipato kwa mujibu wa sheria, pamoja na kujadili mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo yao .Leo nitaomba tujadili kuhusu vikundi vya vijana wenye umri kati ya miaka 15-35, hili ni rika ambalo linachangamoto nyingi sana za kimaisha katika jamii yetu.

kikundi cha vijana cha sanaa cha DEGE LA JESHI katika halimashauri ya wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.

NAMNA YA KUUNDA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI KWA VIJANA
Hatua ya kwanza
ni lazima mtafute vijana kwanza ambao mnalengo la kuunda kikundi chenu yaani vijana mnaofahamiana kitabia, wenye nidhamu na heshima katika kazi, wenye tabia njema kwa jamii inyowazunguka, vijana msio na tabia ya wizi, ubakaji, ulevi na utumiaji madawa ya kulevya, vijana wenye uthubutu na bidii katika kazi.
Kwa kukosa sifa zinazoendane hapo ndipo vijana wengi huwa tunashindwa na kujikuta baada ya miezi miwili kikundi kimekufa. Ni vizuri tukaanza kwa kutambuana kwanza, sisi wenyewe kuwa ni vijana wa aina gani,tunataka kujiunga kwa sababu gani,je sababu tu ni kelele za viongozi kuwa tujiunge kwenye vikundi?.Eneo hili linahitaji fikra na busara sana, mkishindwa hapa huko mbele hakuna litakalofanyika.

kikundi cha vijana cha sanaa cha YOUTH TALENT DEVELOPMENT MKOANI MBEYA

Hatua ya pili
Ni muhimu kikundi kikawa na malengo ya muda mafupi na malengo ya muda mrefu ambayo yamepangwa pamoja na wanakikundi wenyewe siyo mtu mmoja apange kwa niaba ya watu wengine, malengo hayo yaweza kuwa ya miezi mitatu, miezi sita, mwaka na hata miaka mitano kulingana na aina ya shughuli mtakazokuwa mnafanya.
Malengo yakipangwa na wanakikundi wote inakua raisi kutekelezeka kwani kila mtu anaona yeye ni familia ya kikundi kile, lakini mkishindwa kuwa na ushirikiano basi ni vigumu kuyafikia malengo yenu.
Hatua ya tatu
Ni muhimu kutafuta uongozi wa muda kwani hapa ndiyo mahali ambapo uongozi wa muda unatafutwa ili uweze kuratibu na kusimamia shughuli za kuimarisha kikundi, najuwa mpaka kufikia hatua hii kikundi bado kinakuwa kinapitia changamoto nyingi sana wapo watakaoona wanapoteza muda, wapo watakaokua wanajaribu tu kama mtaweza fika mbali n.k
Hatua ya nne
Kuandaa mchakato wa utengenezaji wa katiba ya kikundi, hapa ndipo jina la kikundi hupatikana, malengo na shughuli zitakazofanywa na kikundi hujadiliwa na kwa kina, majukumu ya viongozi watakaochaguliwa yatakua ni yapi, adhabu na mafao ya mwanakikundi, kwa kifupi katiba ndiyo mhimili wa kikundi, ikikosewa hapa ndio dira na muelekeo wa kikundi utakuwa unaenda kombo. Katiba ni lazima ijadiliwe na wanakikundi wote.
Hatua ya tano
 Ni kusajili katiba ya kikundi, ni muhimu katiba ikasajiliwe katika halmashauri husika ili kuweza kufanya shughuli kihalali.
NAMNA YA KUENDESHA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI
i) Kutengeneza katiba iliyobora.Kikundi ni lazima kitengeneze katiba ambayo itatoa muongozo wa namna ya kujiendesha, majukumu ya viongozi na wajumbe wengine wa kikundi. Katiba ya kikundi ni lazima ipendekezwe na wajumbe wengine ili kila kitu kilichomo kwenye katiba kieleweke na kila mjumbe. Sio vizuri na ni mbaya kunakili katiba ya watu wengine na kuifanya iwe yenu kwani vikundi hutofautiana kwa aina ya watu waliopo na shughuli wanazofanya.
ii) Kuwa na uongozi imara.Kikundi ni lazima kiwe na uongozi imara katika kusimamia shughuli mbalimbali za uzalishaji na utawala.Ni muhimu kuchagua viongozi wenye nia na lengo la kufanikisha kikundi kinasonga mbele,usimchague mtu sababu/kiongozi sababu ni ndugu au rafiki yako au mnafahamiana.
iii) Wanakikundi lazima waheshimiane wao wenyewe bila ubaguzi wa aina yoyote ile wa rangi,jinsia,kitikadi,kiuchumi,kuwa na nidhamu ya matumizi ya pesa na mali zingine za kikundi.
iv) Ni lazima maamuzi yanayofanywa ndani ya kikundi yafuate sera,sheria na kanuni zilizowekwa na kupitishwa na wanakikundi wenyewe.Maamuzi yasifanyike kwa kumkandamiza mtu au kikundi cha watu Fulani ndani ya kikundi.
v) Kikundi pia lazima kiwe na mikakati ya kubuni miradi ya uzalishaji mali ambayo ina tija kwa wanachama wake,miradi hiyo yaweza kubuniwa na wanachama wenyewe au kuomba msaada toka kwa wadau wengine wa serikali na mashirika binafsi.Vile vile kikundi lazima kijenge utamaduni wa kuaminiana baina ya viongozi na wanachama wenyewe,kwani hii huongeza mahusiano mazuri baina ya wanachama na kupelekea kikundi kufanikiwa.
vi) Viongozi wa kikundi lazima muwe na utaratibu wa kutafuta taarifa mbalimbali zinazohusu maendeleo ya kikundi,ni muhimu kutafuta taarifa mbalimbali zinazohusu maendeleo ya vijana na stadi mbalimbali za maisha ili muweze kujiendesha kiuchumi na kijamii pia.Kila mwanakikundi awe kiongozi na asiwe kiongozi ni lazima ayaweke maslai ya kikundi mbele kuliko maslai binafsi,ni vibaya kutumia pesa na mali za kikundi kwa kujinufaisha mwenyewe.
vii) Viongozi wa kikundi wanajukumu la kuhakikisha kunakuwa na mgawanyo mzuri wa majukumu kwa wanakikundi na wafanyakazi walioajiriwa ili shughuli zote za kikundi ziweze kwenda kama zilivyopangwa.
viii) Vilevile wanakikundi wanatakiwa kuwa na mtazamo wa mbali na kuweka mawazo yao katika mpangilio mzuri wa kutekelezeka.
ix) Ni muhimu pia kuwa na vikao vya ndani vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria na katiba ya kikundi. Kutofanya vikao kunaweza kuibua maneno baina ya wanakikundi na kukigawa kikundi.
Pamoja na hayo yote,vikundi vingi vya ujasiriamali vya vijana vinakumbwa na changamoto nyingi sana na hivyo kushindwa kuyafikia malengo kama ifuatavyo:

Vijana wengi waliopo kwenye vikundi vya ujasiriamali wana haraka ya maendeleo ya ghafra na kwa muda mfupi, hivyo kushindwa kuendana sambamba na mifumo mbalimbali ya kimaendeleo inayotolewa na serikali pamoja na wadau wengine.Vilevile baadhi ya vikundi kushindwa kushiriki katika vikundi vya kuweka na kukopa pamoja na taasisi mbalimbali za kifedha.
Vikundi vingi vya vijana pia vimekosa taarifa juu ya mifuko rasmi ya vijana ambayo ingeweza kusaidia kuwa chanzo cha fedha kutunisha mifuko yao na hatimaye kuongeza mitaji waliyonayo, lakini pia hata wakizijua fursa hizo bado kuna milolongo na vikwazo vingi vya kuwawezesha kupata fursa hizo. Lakini pia vikundi vingi vimekosa elimu ya namna ya kusimamia shughuli za vikundi na hivyo kupelekea kupoteza dira ya maendeleo.

Tafadhali; Kabla ya kumaliza nitakua mchoyo wa fadhila kama sitozungumza ili,vikundi vingi vya vijana vinavyojishughulisha na ujasiriamali huwa ni vikundi vya mazoea, huundwa kulingana na undugu wa watu Fulani, urafiki Fulani na hivyo kupelekea mambo mengi kufanyika kwa mazoea. Lakini pia vikundi vingi vya vijana vya ujasiriamali vinaanzishwa kwa lengo kuu la kupata pesa au kuwezeshwa na mtu Fulani, na pale msaada unaposhindikana basi hufa mara moja. Hivyo basi ni vyema vijana tunapoamua kuwa pamoja, tunapoamua kuanzisha vikundi vya ujasiriamali ni vyema tukaepuka mambo haya, ni bora mkawa wachache wenye lengo la kujikwamua kiuchumi kuliko kuwa wengi ambao hamna faida yoyote.


Comments

  1. Hongera sana ndugu mwandishi umetisha sana umenkfunza jambo nami pia ningependa kujiunga kwenye kikundi lakini sijapata fursa hiyo

    ReplyDelete
  2. Asante kwa kutufungulia njia kwa kutuelimisha kama vijana Wende future

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi