Skip to main content

MAMBO MUHIMU KIJANA KUYAJUA.

 MAMBO MUHIMU KILA KIJANA KUYAKAFAHAMU KUHUSU YEYE (KIJANA):
1. Ni lazima ujitambue, upate ufahamu sahihi juu ya maisha yako pamoja na mambo yote na jamii inayokuzunguka
2. Ni muhimu ujue wajibu ulionao kwako wewe mwenyewe kama mtu binafsi juu ya maisha yako
3. Kuna haja ya kujua kuwa wewe ni sehemu ya familia yako na lazima ujue wajibu wako kwa wazazi na familia kwa ujumla
4. Ni lazima ujifunze kuwa mzalendo wa taifa lako sawa na jinsi ambavyo Mungu anataka, fahamu kuwa umeunganishwa na ardhi ya Tanzania kwa mafanikio yako, Mungu akikwambia nenda nje ya nchi nenda lakini usifikiri mafanikio hayako Tanzania
5. Kijana anatakiwa ajitambue, ajielewe yeye ni nani na ana kusudi gani katika maisha yake
6. Unatakiwa kupata uelewa wa kutosha juu ya kipindi cha ujana na umuhimu wake ukiwa bado Kijana ili ujue namna ya kuzingatia na kujipanga kwa hapo baadae
7. Kuelewa changamoto zilizopo katika kipindi cha ujana na namna ya kuzishinda kuna uhusiano na namna unavyojitambua ukiwa bado kijana
8. Kujenga shauku, nia na kiu kwa kijana ili aweze kuishi maisha yenye mwelekeo na aweze kutimiza maono yake akiwasaidia na wengine kumjua Mungu na maisha yake kwa ujumla wake
9. Kuwekeza uthamani na nguvu ya kipindi cha ujana kwa mtazamo wa Ufalme wa Mungu
UELEWA JUU YA UJANA NA KIJANA
1.  Ujana ni hatua ambayo mtu anaipitia baada ya utoto au ni kipindi cha kati cha makuzi ya mtu kabla ya utu uzima na hatimae uzee
2.Ujana huanza mara baada ya mtu kubadilika kimaubile na huanzia miaka kumi na mbili wengine hadi kumi na tano ambapo mtu huanza kuwa na hisia za kimwili na kutamani sana kuwa na uhuru wake katika maamuzi. Mabadiliko haya huchochea au qhupelekea hisia mbalimbali za kimwili na mabadiliko ya jumla ya tabia
3.Ujana ni majira yanayopita katika makuzi ya mwanadu, ukifanikiwa kuwa mzee ni lazima ulipita katika kipindi hiki au daraja hili la ujana, kwa hiyo kama bado uko katika dara hili ni muhimu kujipanga ili usije ukajilaumu mbele ya safari
ZINGATIA HII
“Huwezi kuyajali maisha yako kama hujui thamani yake, huwezi kujua thamani ya maisha yako kama hujajitambua kwa Neno la Mungu, huwezi kuwa na maisha ya mafanikio kama maamuzi yako hayatengenezi mafanikio, ufahamu sahihi juu ya maisha yako ndio msingi wa kujitambua kwako, yaani kuijua Kweli ili hiyo Kweli ikuweke huru na ndipo utakapokuwa huru kweli kweli, kumbuka hata usipoamua maisha yako yataendelea kama kawaida. Zaidi ya hayo kama hujui wewe ni nani huwezi kujua thamani yako, kama hujui thamani yako lazima utaishi chini ya kiwango cha maisha unayotakiwa kuishi”
UTAIJUAJE NAFASI YAKO KAMA KIJANA
Nafasi yako kama Kijana ni wajibu wako, umuhimu ulionao kwako na kwa jamii kwa ujumla wake pamoja na familia yako. Lazima ujue Nafasi yako katika maeneo yafuatayo:
• Kwako binafsi,
• Kwa familia yako,
• Kwa kanisa lako,
• Kwa jamii yako
• kwa mkoa wako,
• kwa taifa lako na
• kwa Ufalme wa Mungu. Safari ya kujua
Nafasi yako katika maeno yak ohayo yote inaanzia katika neon moja tu: KUJITAMBUA.
Jenga Ufahamu Hapa
1. Kujitambua ni hatua ya muhimu katika maisha ya mtu yoyote duniani kama anataka kuishi kwa Furaha na matumaini na kufikia malengo yake
2. Kujitambua ni matokeo ya kupata ufahamu sahihi juu eneo fulani utakaokusaidia kufanya maamuzi sahihi katika eneo husika ili uweze kufanikiwa
3. Ufahamu au maarifa unapatikana kwa kutafuta, kuchunguza na kudadisi taarifa mbalimbali kwani si kila namna ya kujitambua ni sahihi kwa kijana
4. Matokeo ya ufahamu ulionao yatafanana na ubora wa maisha unayoishi kwa kiwango cha kuathiri maamuzi yako ya kila siku
5. Kiwango cha matokeo ya kujitambua kitafanana na ubora wa taarifa ulizozipata
6. Udhihirisho wa maisha ya kujitambau ni hatua ya juu kabisa ya kuthibitisha kwamba kweli umejitambua


Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi