Skip to main content

ONDOKANA NA UTUMWA HUU

Image result for MIND PICTURES


Nikusihii kitu kimoja mpenzi msomaji wa makala hizi za YAPOCODE TANZANIA kwamba maisha ambayo unaishi muda mwingine jua ni kwasababu ya utumwa ambao umeujenga katika fikra zako.Huu utumwa ambao umeujenga katika akili zako ni utumwa ambao umekufunga kufikiri vizuri juu ya maisha yako,ni utumwa ambao umekufanya kujiona huna thamani mpaka mtu flani akufanyie kitu flani ndipo ujione kwamba unathamani katika maisha yako.Mpaka lini utaogopa kufanya unachotaka kukifanya kwasababu mtu flani kafanya kitu kama kacho ambacho unaogopa kukifanya,lini utaacha uwoga wa kuwa mtu mnyenyekevu hata kwenye sehemu ambazo zinahitajjuhudi zako kuwa zaidi ya unyenyekevu sehemu ambazo sio? lini utasema sasa najijenga mwenyewe na niweze kuwa zaidi ya leo nilipo?. Nakusihii usiache utumwa wako wa kifikra kuacha lulu iliyoko ndani yako kupotea,usiache utajiri ambao uko ndani yako kupotea.leo hii anza na jitahidi kufanya kile ambacho unaogopa kukifanya lakini unajua kabisa kwamba ni kitu chema katika maisha yako.

Nimeshakutana na watu wengi sana ambao wanakuwa watumwa wa kifikra katika maisha yao kwasababu wanaogopa watu flani watawaambia kitu gani ikiwa wataamua kuchukua hatua nzuri za maisha yao.Nasikitika sana kumwona Lionel Richie wa kitanzania anaishi kama kuku anayefugwa ikiwa anaweza kutumia sauti yake kuimba na akatikisa Dunia, nasikitika kumwona Warren Buffet wa kitanzania akiishi maisha kama ya mtu ambaye hana ramani yoyote ya maisha yake ikiwa ana akili na mwili ambavyo anaweza kuvitumia na kupata hela ya kuwekeza katika biashara,nasikitika kumwoma Mmbwana Sammata kutoka sehemu zingine za Tanzania ana smartphone nzuri lakini anakuwa ni mtu ambaye hajui alichokuwa nacho ikiwa anaweza kutumia YOUTUBE,FACEBOOK,INSTAGRAM kuweza kujitangaza kwa kipaji alichokuwa nacho na akapata nafasi za kusonga mbele kimataifa,nasikikita sana nikimwona Mrisho Mpoto katika sehemu zingine za Tanzania lakini anaogopa kuimba kwasababu watu watamcheka. Nazidi kuvuta picha kwa wadada na wanawake kwamba nasikitia nikimwoma Ophrah wa kitanzania akiogopa kutumia sauti yake na ujasiri wake kwasababu anaona tayari kuna watu bora zaidi yake, nasikitika nikimwona Mama Alaska mwingine wa Kitanzania katika maeneo mengine Tanzania anayeogopa kuthubutu kwasababu anaona Mama Alaska tayari yupo,nazidi kusikitika kumwona  mwanamke mwenye kipaji cha uhubiri na kufundisha neno la Mungu zaidi kama Joyce Mayer lakini anaogopa kuomba nafasi kufundisha wenzake kanisani na hata kwenye mitandao ya kijamii.
Leo ni mwisho kwa ufungwa huu wa kutokutumia ulichokuwa nach,leo hii iwe ni siku ya kusema utumwa huu ambao unasababisha umasikini katika maisha yako sasa baasi.

Kama bado hujajiunga na program ya akili ya ushindi jitahidi sana kupata maelezo haya kwa kubonyeza http://www.akiliyaushindi.com/jiandikishe

Ulikuwa nami;

Kocha Lazaro Samwel
0753616584
EMAIL; lazarosamweli41@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi