Skip to main content

KAMPENI YA BINTI JITAMBUE TANZANIA

MHUTASARI KUHUSU MRADI
Katika uzinduzi wa kampeni hii ya Binti Jitambue ni moja ya utekelezaji wa malengo 17 ya malengo ya milenia ambayo yaliafikiwa na wanachama 189 wa umoja wa Mataifa mwaka 2015, ambapo lengo  namba 3  linazungumzia haki sawa kwa wote na kumwezesha mwanamke (Promote Gender Equality and Empower Women). Ukiachilia mbali malengo ya milenia hata shiriki letu la YOPOCODE malengo yake yako bayana juu ya kumsaidia kijana kujitambua Na hii inaenda sambamba kabisa na kampeni yetu ya “ BINTI JITAMBUE”.Hivyo tunaamini kampeni hii itakuwa ni chachu ya maendeleo kwa vijana wa kike. Na kwa mwaka 2017/2018 tutaanza na kata 18 za Halmashauri ya Mbeya vijijini na baadaye kampeni yetu kusambaa mkoa mzima na taifa kwa ujumla wake.

VIASHIRIA
Kuna viashiria mbalimbali ambavyo vimepelekea kuanzisha kampeni hii ya binti jitambua
1. Kuwepo kwa wasichana ambao wanaacha shule kwa sababu ya kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi ,hii inatokana na wasichana wengi kukosa elimu ya kujitambua na kufanya maamuzi sahihi hasa pale anapokutana na vishawishi
2. Kuongezeka kwa idadi ya wasichana wanaopata mimba wakiwa shule .
3. Wasichana kukosa elimu ya ujinsia kabla na baada ya kuvunja ungo.

MALENGO YA MRADI
Malengo mahususi ya mradi huu ni kuwafikia mabinti 900 katika Halmashauri ya Mbeya vijijini KUWAJENGEA UWEZO KUHUSU ELIMU YA KUJITAMBUA.

MALENGO YA JUMLA
Malengo ya kampeni hii ya Binti Jitambue yanatokana na changamoto mbalimbali ambazo mabinti wengi wanapitia katika kipindi cha ukuaji na mabadiliko ya miili yao ambayo hutokea baada ya kuvunja ungo.
Hivyo malengo yafuatayo yataweza kumwezesha binti kutambua na kuchukua hatua kufanya maamuzi sahihi.
1. Kuwa na taarifa sahihi za mabadiliko yanayotokea katika mwili wake. Hii itamwezesha binti kujua ni wakati upi na ni nini cha kufanya anapoona mabadiliko fulani katika mwili wake. Kwa sababu atakuwa na taarifa sahihi hivyo, ataweza kuchukua hatua impasayo na kwa wakati sahihi.
2. Kutoa  elimu ya kujitambua na kujiepusha na vishawishi kutoka kwa wanaume
Wasichana wengi hukumbana na vishawishi kutoka kwa wanaume ambavyo husababisha kushindwa kuendelea na masomo kwa kupata mimba, pia kuingia kwenye ngono zembe ambayo huwafanya kutumia muda mwingi kujihusisha na mapenzi badala ya kusoma. Hivyo tunaamini kampeni utawapa uwelewa wa kutosha kuhusu njia mbalimbali za kuwaepuka mafataki huko mitaani
3. Kujumuika na makundi rika
Elimu kuhusu makundi rika itawawezesha vijana/mabinti kutambua nafasi yake katika kufanya maamuzi kwani wengi wao hufuata mkumbo kutoka kwenye makundi rika elimu hii itawaongezea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi na kwa wakati sahihi.
4. Kuchagua marafiki
Tunatambua kwamba kila msichana huwa na rafiki yake ambaye anamwamini na kumweleza mambo yake yote, elimu ya kumwezesha binti kuchagua rafiki mwema. Hii  itawafanya mabinti kuwa na marafiki watakaowaongoza kufikia malengo yao.
5. Kuwawezesha wasichana kuwa na malengo.
Wahenga walisema huwezi kupotea kama hujui unapokwenda, kama wasichana watapatiwa elimu ya namna gani ya kupanga malengo na kuyafikia malengo ambayo ameyapanga.
6.    Kuongozwa ili ajenge haiba.
Elimu kuhusu haiba itawawezesha mabinti kuwa nadhifu katika mavazi na miili yao pia. Kwani kumekuwa na kasumba hasa kwa mabinti kuvaa nguo za ajabu(nusu uchi) na hivyo kuongeza ushawishi kwa wanaume hasa mafataki au wanaume wasio na hofu ya Mungu. Kwa mabinti wadogo wenye umri sawa na watoto wao.

UHAI WA MRADI:
YOPOCODE  kwa mara kadhaa tumeshiriki katika kampeni za kijamii na kwa uzoefu tulio nao miongoni mwetu viongozi inatupa imani na nguvu kuwa mradi huu pekee utadumu na kuwanufaisha walengwa kwa kiasi kikubwa. Mwaka 2016 miongoni wa viongozi wetu walishiriki katika kampeni ya LISHE YA MAMA NA MTOTO iliyokuwa inafanyika mkoa wa Lindi chini ya shiriki la maendeleo ya wanawake ROWODO na kudhaminiwa  na shirika la kimataifa la  SAVE THE CHILDREN..

WADAU WAKUU WA KAMPENI/MRADI
Ili kampeni hii ya BINTI JITAMBUE iweze kuwafikia wasichana wengi zaidi na jamii  kwa ujumla wake, tumependekeza wafutao kuwa wadau wa kampeni hii na mchango wao unahitajika sana kufanikisha mradi wetu;
a)      Mkuu wa mkoa wa Mbeya
b)      Wakuu wa wilaya ( kwa sasa mkuu wa wilaya ya mbeya)
c)      Maafisa elimu wa mkoa na wilya
d)      Maafisa maendeleo mkoa na wilaya
e)      Maafisa ustawi mkoa na wilaya
f)       Viongozi wa dini na siasa
g)      Wakuu wa shule za misingi na sekondari
h)      Wanafunzi wa kike kwa shule ya msingi kuanzia Darasa la tano hadi la saba
i)        Wanafunzi wa sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita.

NAMNA YA KUFIKISHA UJUMBE WA KAMPENI
BINTI JITAMBUE ni kampeni iliyoandaliwa mahususi kuwasaidia watoto wa kike/ binti kukuza uelewa na kujitambua na hatimaye kufikia malengo kielimu na kimaisha kwa maslahi ya maisha yao na jamii nzima. Kwa hiyo ili kuhakikisha ujumbe wa kampeni unaifikia jamii ya Tanzania na walengwa yaani wanawake ( binti) tutatumia vyombo vya habari kama ifuatavyo;
a)      Mitandao ya kijamii kama facebook, whatsapp na blogs
b)      Radio naTelevision kwa matangazo na mahojiano
c)      Vipeperushi na mabango
d)      Magazeti na majarida
e)      Mbao za matangazo za mashuleni
i) Aidha tutaanzisha klabu za wasichana mashuleni zenye lengo la kuwafanya wapate mwamko wa kujadili kwa pamoja changamoto zao kupitia midahalo na mijadala yao.
ii) mashindano ya mpira wa pete na miguu kwa timu za wanawake.

iii) michezo na burudani zitakazowafanya wakutane na kujenga urafiki miongoni mwao.

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi