Skip to main content

BARUA YA NANENANR

YOUTH POTENTIALS FOR COMMUNITY DEVELOPMENT (YOPOCODE)      
SIMU: +255-758 051641,+255-768 577408,0765300255,0653983001, 0768416619
Barua Pepe: yopocode@gmail.com
KWA MADIWANI WOTE WILAYA YA MBEYA VIJIJI/VIONGOZI
WA VIKUNDI/TIMU/BENDI NA MTU MMOJA MMOJA
YAH: MWALIKO WA KUSHIRIKI KATIKA TAMASHA LA NANENANE 2017 LITAKALOFANYIKA VIWANJA VYA ILEMBO MBEYA VIJIJINI.
Rejea kichwa cha habari hapo juu kama kinavyojieleza. Shirika la vijana Tanzania la  Youth Pontential for Community development( YOPOCODE)” linakuletea Tamasha La Nanenane 2017 litakalofanyika katika viwanjwa vya shule ya msingi ya Ilembo Mbeya Vijiji kuanzia 01/08/2017 hadi 08/08/2017.Lengo la tamasha hili ni kuwahamasisha vijana kushiriki katika shughuli za maendeleo ikiwemo kilimo ili kuinua maisha yao kiuchumi. Pia kuhamasisha vijana kujali na kulinda afya zao kwa kushiriki michezo na burudani mbalimbali zenye tija na kukuza na kuendeleza vipaji kwa vijana Tanzania.Ili kufanikisha tamasha hili kwa ubora zaidi shirika limeaandaa utaratibu ufuatao na kuteua vipengelee kadhaa ambavyo vitashirikishwa katika tamasha letu. Aidha tumeanishi vigezo hapo chini:
Aina Ya Kipengele
Kiingilio
Zawadi Kwa Mshindi wa (kwanza,pili na tatu)
Ngoma Za Asili
10,000/=
(I)100,000/=,(II)50,000/= (III) 20,000/
Mpira Wa Miguuu
20,000/=
I)Ng’ombe Na Mpira (II) Mbuzi Na Mpira Iii)Mpira1
Muziki/injiri/bongo/dansi
10,000/=
(I)100,000/=,(II)50,000/= (III) 20,000/
Midahalo
10,000/=
(I)100,000/=,(II)50,000/= (III) 20,000/
Maonyesho Vya Kilimo
10,000/=
(I)100,000/=,(II)50,000/= (III) 20,000
      ZINGATIA: Kwa upande wa mpira wa miguu tuanze mapema tarehe 26/05/2017 ligi kwa ngazi ya kata kwa kila kata na mshindi wa kwanza ndiye atayeingia fainali itakayofanyika Ilembo mbeya vijiji. Kupata fomu ya ushiriki piga simu au fika ofisini Ilembo madukani.aidha kwa vikundi vya ngoma, kwaya na wasanii wa kujitegemea tuanze maandalizi mapema sana ili tuweze kujizolea zawadi kiabao.
Alfred Sostern Mwahalende
Mkurugenzi mtendaji
YOUTH POTENTIALS FOR COMMUNITY DEVELOPMENT

                                  

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi