Skip to main content

VIJANA NA UCHUMI

                                         VIJANA NA UCHUMI

Vijana,vijana,vijanaaaaaaa ndio imekua mada moto sana katika vichwa vya watu wengi sana hapa Tanzania na Duniani kwa ujumla.Lakini imekua tofauti miongoni mwao kwani wapo baadhi waliojitambua ya kuwa wao ni vijana na wanatakiwa wafanye nini,ila wapo ambao wametambua wao ni vijana na wameshindwa kujua wafanye nini,wengine kwa makusudi kabisa na kubaki kuwalalamikia wazazi na serikali kwa ujumla ya kuwa wamewatenga.
Je,kijana ni nani?ni mtu ambaye yupo kati ya miaka 15 mpaka 35,kwa mujibu wa malengo ya maendeleo endelevu toka umoja wa mataifa,wanasema karibia nusu ya idadi ya watu duniani wapo chini ya miaka 25,manake vijana tunaendelea kuwa wengi duniani.
Lakini hiyo haitoshi,90% ya watu ambao wapo chini ya miaka 25 wanatoka kwenye nchi zinazoendelea na Tanzania tukiwa miongoni mwao.pia zaidi ya 67% ya watanzania wote ni vijana hii ni kwa mujibu wa sense ya mwaka 2012.Hii naweza sema kuwa sisi vijana ni rasilimali kubwa inayotegemewa na taifa letu lakini na dunia kwa ujumla.

Vijana tumekua watu wa maongezi na wapangaji mikakati mingi pasipo kuitekeleza kwa vitendo na hivyo kupelekea kupishana na fursa nyingi zinazojitokeza kwa vijana katika ulimwengu huu ambao kila kona kijana amekua ni mada kuu katika mazungumzo.

Vijana tumekua watu wa matumizi mengi kuliko hata vile tunavyoingiza kama kipato,inafikia hatua mpaka mtu anakopa kwa ajili ya kufanya anasa na starehe zingine za dunia,tumeshindwa kuwa na mikakati endelevu ya kufanya uzalishaji ili tuweze kulisongesha taifa letu mbele na badala yake kutumbukia kwenye dimbwi la starehe tu na kushindwa kuwaza,kubuni na kufanya vitu vya msingi.

Kutokana na ukweli huo,vijana tunatakiwa kuwa wepesi wa kujifunza na kufanya mambo kwa uharaka na ubora unaohitajika.Ni lazima tuwe wabunifu katika masuala mbalimbali ya maendeleo,vijana lazima tuwe wabunifu katika kutafuta mawazo ya kufanya biashara,uwekezaji,utafutaji wa masoko.Mfano vijana mnaweza pata mtaji kwa kuwa kwenye kikundi na mkacheza vikoba au mkaomba mkopo nafuu toka halmashauri husika.
Ni muhimu kuwa wabunifu katika kutafuta mitaji mbalimbali kwa kuzitambua na kuzitumia rasilimali tulizonazo ili ziweze kuwa na mnyororo mkubwa wa maendeleo ya taifa letu,lakini ikumbukwe kuwa ubunifu huu uendani na uwezo wa kukabili changamoto zitakazojitokeza katika shughuli zetu.

Uchumi na vijana ni namna vijana tunavyoweza kupambanua uwezo na udhaifu,ujuzi na maarifa ya namna ya kumiliki uchumi wetu,nchi na dunia kwa ujumla,kwa kuangalia maeneo gani ya uhitaji katika nchi ili sasa uwekezaji wetu uweze kuwa na tija na endelevu.

Uchumi ni nini?
Uchumi ni jumla ya kazi au shughuli ambazo mtu,kikundi cha watu,serikali wanafanya ili kutosheleza mahitaji ya bidhaa au huduma Fulani katika kijiji,kata,wilaya,mkoa,kanda na nchi kwa ujumla.

Shughuli hizo zaweza kuwa za uzalishaji na usambazaji wa bidhaa Fulani,utoaji wa huduma halali ili mradi pesa au mapato yanapatikana.Kuna maeneo ambayo mimi nayaona ni fursa kwetu vijana kama tutaweza kuyatilia mkazo na kuyapangia mikakati ya maksudi.maeneo kama kilimo na viwanda yameonekana kuwa manufaa kwetu.
Serikali yetu imeonesha nia ya dhati ya kutupeleka kwenye uchumi wa viwanda hasa ukiangalia kwenye bajeti ya mwaka huu 2016/17, kwani inakadiriwa zaidi ya 40% imetengwa kwa ajili ya maendeleo hususani katika ya sekta ya nishati na madini hii inamaana kutakuwepo na mapinduzi ya umeme na kupelekea sekta ya kilimo na viwanda kuwa na tija.

Ni lazima vijana tuanze kuwekeza katika viwanda vidogovidogo hususani katika usindikaji wa mazao yatokanayo na kilimo,hii itatupelekea kuongeza thamani mazao hayo na hivyo kutoa ajira kwa makundi mengine yanayojishughulisha na kwani masoko yatakua yamepanuka kwa upande wao.

Mfano baada ya serikali kuonesha nia ya ujenzi wa kiwanda cha kusindika zao la muhogo mkoani lindi kinachokadiriwa kugharimu zaidi ya billion 1.3 za kitanzania,vijana wengi baada ya kuelimishwa wameanza kujiingiza katika kilimo cha muhogo ambacho baada ya muda mfupi itakua lulu kwa maendeleo yao.

Vile vile vijana lazima tuwe na maono ya mbele katika masuala mbalimbali ya kiuchumi,nakuna kuna kikundi cha vijana mkoani lindi pia kinaitwa Zinduka kinahamasisha jamii juu ya ufugaji wa kuku na wanyama wengine,lakini wao wanamalengo ya kuanzisha mashine ya kukoboa na kusaka nafaka,lakini pia utengenezaji wa chakula cha wanyama.
Hii yote ni kuwa baada ya uhamasishaji kwa jamii juu ya ufugaji,wao watanufaika kutokana na ongezeko na uhitaji wa chakula cha mifugo hiyo.hii kuonesha tu kwamba ubunifu na maono ni silaha pekee ambayo itatutoa kutoka kwenye dimbwi la umasikini tulionao.

Kwa kifupi ni kwamba vijana tutakua tumeshiriki moja kwa moja katika kukuza uchumi wetu hii ni kutokana na sababu zifuatazo;
Moja,tutakua tumeongeza pato la taifa hii ni kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa sokoni ambazo zitatakiwa kusajiliwa na kuanza kulipa kodi.Lakini pia tutauza bidhaa nje ya nchi na hivyo kuongeza wigo wa soko letu kutokana na bidhaa zilizofungwa vizuri na zenye ubora baada ya kupata mafunzo mbalimbali.

Pili, tutakua tumepunguza tatizo la ajira kwa vijana wenzetu kwani viwanda na mashamba ambayo tutakua tumewekeza tunatarajia watu watakua wameajiriwa huko.
Tatu,Tutakua tumepunguza mfumuko wa bei unaotokana na kuingiza bidhaa nyingi toka nchi nyingine,hii ni kutokana na kuongeza uuzaji wa bidhaa nje ya nchi(exportation) na kupunguza uingizaji wa bidhaa ambazo tunauwezo wa kuzalisha wenyewe hivyo kupunguza bei ya bidhaa kuwa kubwa nchini(import inflation).

La mwisho,tutakua sehemu ya kuifanya shilingi yetu iwe imara kwa kuongeza fedha za kigeni nchini kutokana na uuzaji wa bidhaa nje ya nchi.
Hivyo basi nchi yoyote duniani ili iendelee ni lazima ianze na rasilimali watu ambao wengi ni vijana,na lazima sisi tushirikiane na serikali tuwe mstari wa mbele kuongeza uzalishaji wenye tija mana ndio tuna nguvu kushinda makundi mengine ya umri.
Ni lazima tuwekeze nguvu katika kutafuta maarifa ili yatujenge na kutusaidia katika maisha yetu ya kila siku,tusiwe vijana wa kulalamika tu,tuwe vijana wa kufanya kazi kwanza,vijana ni muhimu kuwa na ndoto,mikakati ya kuzifikia ndoto zetu,huwezi kupanda bangi na ukategemea kuvuna mpunga .

Ni wajibu kujua kwamba,kabla hujamlaumu kiongozi wako,mzazi wako ya kwamba hajakufanyia kitu,jaribu kujiuliza wewe hiyo elimu yako,nguvu zako,uzuri wako umeifanyia nini jamii inayokuzunguka hata kwa ushauri tuu.
Vijana lazima tuwe mabalozi wa maendeleo kwani tuna nguvu na uwezo wa kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja,maarifa na ujuzi tulionao ni tunu kwa taifa letu hivyo hatuna budi kutumia katika misingi ya uadilifu na unyenyekevu kwa maendeleo yetu na taifa kwa ujumla

NIMALIZE KWA KUSEMA
HUWEZI KUBADILISHA MAMBO, KWA KUPAMBANA NA UKWELI ULIOPO.
FILBERT NYONI
MSHAURI MASUALA YA UCHUMI NA UJASIRIAMALI
MSHAURI MASUALA YA MIRADI YA KIMAENDELEO NA USIMAMIZI WAKE
MJASIRIAMALI CHIPUKIZI
MWEZESHAJI BIASHARA-MRADI WA ELIMU FURSA, LINDI


Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi