Skip to main content

KIJANA NI NANI??

DIRA YA MAISHA YA KIJANA

Kijana ni nani?
Ø  Neno kijana linatafsiriwa katika tafsiri tofauti katika kila jamii, Mathalan nchini Tanzania kijana ni mtu mwenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 35, yaani baada ya balehe. Mabadiliko makubwa ya kimaumbile hutokea sambamba na kukomaa kwa mawazo.
Ø  Aidha Kwa mujibu wa sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15 hadi 24.
Ø  Hali kadhalika Kwa tafsiri ya umoja wa mataifa, Kijana ni mwanamke au mwanamme aliye na umri kati ya miaka 15 hadi 24. Tafsiri hii hutofatiana kutoka nchi moja hadi nchi nyingine. Nchi au maeneo mengine ya dunia huwa na tafsiri tofauti kulingana na mahitaji ya mazingira na maeneo yao, na pengine kwa mujibu wa mifumo ya kijamii,kisiasa na kisheria katika nchi hizo.
Ø  Ni kipindi cha mpito kutoka utoto kuelekea uzee.Ni kipindi chenye heka heka nyingi kwa vijana kutokana na mabadiliko ya kimaumbile, kwani kijana hutaka kujionyesha kwamba yeye ni nani katika jamii.
Kwa kweli na hapa ndiyo msingi wa maisha ya uzeeni.Na pia ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa kwani vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa.
Ø  Katika taifa lolote lile, vijana ni nguzo muhimu katika shughuli na masuala mbalimbali, iwe ni shughuli za ujenzi, vita, siasa, uchumi, utawala n.k. Vijana wana hamu, shauku, ndoto na matumaini makubwa ya maendeleo, huku wakiwa na nguvu nyingi na akili zao zikiwa zinachemka.
NAFASI YA VIAJANA KATIKA UJENZI WA JAMII NATAIFA
1.    Vijana wanapaswa kuwa na fikra yakinifu. Ufikiri yakinifu ni suala muhimu sana kwa vijana. Ufikiri yakinifu ndio hupelekea uvumbuzi na ubunifu wa vitu na mambo mbalimbali. Kama ambavyo John F. Kennedy, Rais wa Marekani miaka ya 1961 - 1963, aliposema "usifikirie kuwa nchi yako itakufanyia nini, ila fikiria utaifanyia nini nchi yako".Hii inamaanisha kuwa vijana wanatakiwa kuja na mawazo mapya yenye maendeleo chanya kwa taifa. Vijana watakuwa wadau wazuri na viongozi bora wa taifa, endapo watakuwa wanajua mambo mengi hususani yanayohusiana na maendeleo, jambo ambalo linahitaji kujifunza kupitia kujisomea kwa kila siku.
2.   Vijana wanapaswa kuwa wabunifu. Gurudumu la maendeleo la taifa lolote, hutegemea sana ubunifu na uzalishaji wa vijana wa taifa hilo. Hii inamaanisha kwamba, taifa ambalo vijana wake hawafikiri, si wabunifu na ni wavivu katika uzalishaji mali, taifa hilo kamwe haliwezi kuendelea. Kila kona ya nchi kwa sasa, vijana wengi wanalia na tatizo la ajira, jambo ambalo nakubaliana nalo kwa asilimia mia moja. Lakini kwa upande mwingine vijana wanapaswa wakumbuke kanuni ya kwanza ya mwendokasi ya Isaack Newton inasema, "hakuna kitu kinachoweza kujongea kutoka sehemu moja kwenda nyingine, pasipo kutumika nguvu". Tafsiri ya kanuni hii, inaweza kuwa inakatisha tamaa hasa kwa wale wanasubiri kuajiriwa. Lakini huo ndio ukweli. Huu ni muda wa vitendo. Ni muda muafaka wa vijana kupanua wigo wa kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa taifa, kwa kufanya ujasiriamali, kilimo, au ufudi stadi. Vijana hawapaswi kusubiri hadi wawe na mtaji mkubwa ili kuanzisha biashara. Wanaweza kuanza biashara kwa mtaji mdogo wa fedha, ambapo kutokea hapo wanaweza kukuza mitaji yao na hatimaye kuzifikia ndoto zao. Kuwekeza na kufanya biashara katika sekta zinazoajiri na kuleta faida kubwa kama sekta za kilimo, viwanda, usafirishaji na mawasiliano.
3.   Vijana wanapaswa kuwa chachu ya mabadiliko. Vijana ni lazima wawe chachu ya mabadiliko. Na mabadiliko hayo hayana budi kuanzia kwao. Ni lazima watumie uwezo wao kuisaidia serikali katika kutekeleza sera zake, lakini pia lazima wapinge kwa nguvu zote aina zote za unyonyaji unaofanywa na mtu au kundi la watu dhidi ya umma, na pia hata unyonyaji unaofanywa na kundi kubwa dhidi ya kundi dogo au mtu mmoja.
4. Vijana wanapaswa kuonyesha mfano mzuri wa aina ya uongozi yenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho. Vijana ni lazima washiriki katika kufanya maamuzi kwa kujiunga na kushiriki katika siasa. Kada ya uongozi ilikuwa imetawaliwa kwa kiasi kikubwa na wazee ambao walidhani kuwa suala la kujenga na kulitumikia taifa, ni jukumu lao na si la vijana, kwa madai kuwa vijana ni taifa la kesho. Lakini hiyo kesho mara nyingi ilikuwa haifiki. Kauli na misemo kama hii imewafanya vijana wakae pembeni na kuacha kushiriki pamoja na kutimiza majukumu yao wakidhani kuwa muda wao wa kutimiza majukumu kwa taifa bado. Taifa lenye vijana wanaojitambua, ni taifa litakaloendelea, na taifa lenye vijana wasiojitambua ni taifa lenye safari ndefu ya maendeleo. Vijana wengi wamedhihirisha kuwa wanaweza kuwa viongozi wazuri au kuwa na mchango mkubwa katika taifa, ili hali wana umri mdogo. Mfano Mwl. Nyerere, alianza kuongoza harakati za kudai Uhuru akiwa na miaka 30, na akaanza kuhudumu nafasi ya Urais wananchi akiwa na miaka 39. Salim Ahmed Salim alihudumu kama balozi wa Tanzznia nchini Misri akiwa na miaka 22. John Samuel Malechela alihudumu kama balozi wa Tanzania kuwakilisha Umoja wa Mataifa akiwa na miaka 28, huku Jenerali Mrisho Sarakikya alikuwa Mkuu wa Majeshi akiwa na miaka 30. Bila kumsahau Hayati Edward Moringe Sokoine, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa vipindi viwili tofauti. Vijana hawa wote walihudumu nafasi zao kwa weledi na uwezo mkubwa.
5. Vijana wanapaswa kuwa na uzalendo kwa taifa lao. Kwa sasa, uzalendo ambayo ni tunu muhimu sana, imepotea miongoni mwa vijana wengi. Ili taifa liweze kustawi, ni lazima watu wake wakiwemo vijana, wawe na mapenzi ya dhati na yasiyo na mipaka kwa taifa lao. 
Maovu yote yanayofanyika katika taifa hili, kama vile rushwa ufisadi, ukwepaji kodi, utakatishaji fedha, na mengine mengi, ni matokeo ya kukosekana kwa uzalendo. 
Kama vijana wa kitanzania, uzalendo ni lazima uonekane katika maisha yao ya kila siku. Uzalendo unapojengeka ndani ya mioyo na akili za vijana wa kitanzania, itawafanya vijana hao waone kuwa Tanzania ni mali yao, na hivyo ni jukumu lao kuilinda.
 Watatumia nguvu zao, akili zao na ujuzi wao kulijenga taifa lao kwa maslahi ya kizazi chaleo na kesho. Kama vijana watakuwa wazalendo, wataweza kupinga rushwa na aina zote za uhujumu uchumi, na hata siku wakipewa dhamana katika ofisi za serikali au taasisi binafsi, wat aendelea kuyapinga maovu.


6. Vijana wanapaswa kufanya kazi Kwa bidii. Vijana ni kama injini ya gari.Bila injini, gari haliwezi kutembea.Vivyo hivyo, taifa bila vijana, haliwezi kuendelea. Kundi la vijana ni uti wa mgongo wa taifa. Vijana ni injini ya uzalishaji na maendeleo, kwa kuwa ndiyo nguvukazi katika uzalishaji wa mazao, bidhaa au huduma. ⁠⁠ Hivyo wanapaswa kuwa wepesi wa kujifunza, kufanya kazi katika mazingira magumu na yenye presha, na kuleta mafanikio makubwa katika taasisi au taifa.
7. Vijana wanapaswa kuwa mabalozi wa kusambaza habari mbalimbali zinazohusu maendeleo. Ni lazima kuwe na taasisi za vijana ambazo ni kubwa na zenye nguvu, ambazo zitakuwa ni majukwaa ya vijana kujihusisha na shughuli za ujenzi wa Taifa ikiwa ni pamoja na kuelimisha jamii kuhusu maendeleo ya taifa lao na Tanzania ya lwo na kesho.

Lakini kwa upande mwingine pia, serikali na jamii kwa ujumla pia haipaswi kukaa nyuma katika kuwajengea vijana katika kuchangia kuleta maendeleo maendelevu. Vijana wanatakiwa kufundishwa maarifa na ujuzi unaoakisi maendeleo ya taifa husika. 
Pia vijana wanapaswa kujua kusoma, kuandika, kufikiri, kuchambua na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taifa hilo. Baba wa taifa la Afrika Kusini, Hayati Nelson Rolihlahla Mandela (Madiba), alipata kusema kuwa "hakuna taifa linaloweza kuendelea, pasipo na kuelimika kwa watu wake".

Nguvu na upeo wa akili za vijana, ni kama tochi inayomulika maendeleo ya Taifa. Katika dunia ya leo, maarifa na ujuzi ndio vimekuwa sarafu (fedha) ya dunia nzima. Lakini hakuna benki kuu ya sarafu hii, bali ni viongozi na jamii ndio hupanga jinsi ya kuzalisha sarafu hii, na jinsi ya kuitumia. Taifa linaweza kuwa na utajiri wa rasilimali kama gesi asili, madini au mafuta, lakini rasilimali hizi zinaweza kuwa hazina maana endapo faida inayotokana na rasilimali hizo, hazitawekezwa katika sekta muhimu kama elimu ambayo ndio shamba la fikra mpya.
Pia ni lazima taasisi zetu za elimu, hususani vyuo vya ufundi, vyuo vya kati na vyuo vikuu, viwaandae wahitimu wao kuwa watengeneza ajira na siyo kuwa wanasubiri kuajiriwa. Kijana anapoanza masomo ya chuo, anapaswa kujua kuwa atakapohitimu hapaswi kufikiria kuajiriwa au kurudi nyumbani na kuwategemea wazazi.

Nchi yetu kwa sasa imeathiriwa sana na siasa, hususani zisizo na tija. Wito wangu kwa wanasiasa wote ni kuwa, wanapaswa watambue kuwa wana jukumu la kuwajenga vijana, na siyo kuwatumia kwa maslahi yao binafsi kama vile kuwashawishi kufanya vurugu, maandamano yaliyo kinyume na sheria, n.k.
Mwisho, Kuna misemo inayosema kuwa "ukishindwa kupanga, unapanga kushindwa" na mwingine ukisema "vijana ni taifa la leo na kesho". Kama kweli vijana ni taifa la leo na kesho, basi leo ndio muda muafaka wa kuliandaa hilo taifa. Na kama tutashindwa kupanga kuliandaa leo taifa la kesho, basi tutapanga kushindwa katika taifa la kesho.

NAFASI NA MAJUKUMU YA VIJANA KATIKA UCHUMI NA MAENDELEO YA TAIFA 
Serikali na Jamii ya Watanzania tunalo jukumu la kuwajengea Vijana uwezo wa kuwawezesha kuwa Viongozi wa baadaye.
Vijana wanatakiwa kuwa wenye maono na ubunifu katika kukuza Uchumi wa Taifa. Vijana wanapaswa
· Kuwa na mawazo mapya, mbinu mpya na kuwa chachu ya mabadiliko chanya ya kimaendeleo; Vijana wanatakiwa kuwa Wajasiriamali wazuri wenye ujuzi mbalimbali (Young Enterprenuers Skills), na
· Kuwa Wavumbuzi wa vitu mbalimbali vitakavyoweza kukuza uchumi wetu; Vijana wanatakiwa kuwa na mahusiano chanya na marafiki wa Mataifa mengine katika Nyanja
· Mbalimbali za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni, kama vile Michezo, Sanaa na Tafiti mbalimbali za Kimaendeleo;  Vijana wanapaswa kuwezeshwa, kupewa nafasi waonyeshe vipaji vyao na kushirikishwa katika shughuli
· Mbalimbali za Uchumi na Jamii kwa ujumla;  Vijana wanapaswa kushiriki katika Uongozi;
·  Vijana wanapaswa kupata elimu bora.


HISTORIA INAONYESHA NI VIONGOZI VIJANA NDO WENYE UWEZO WA KUFANYA MABADILIKO YANAYOTEGEMEWA NA VIJANA WENZIO.
Yesu kristo alianza shughuli zake rasmi akiwa na miaka 30 tu, na mpaka leo kila mmoja anakubali mafanikio ya kazi yake iliyodumu kwa takriban miaka mitatu hivi
Julius ceaser mwasisi wa roman empire akiwa na miaka 29 tayari alishafanikiwa kutengeneza taifa kubwa na lenye nguvu la roma, pia kuasisi milradi mikubwa iliyosaidia vijana wa roma kuwa na nguvu kiuchumi na kijeshi.
Alexander the great akiwa na miaka 30 tu tayari alishafanikiwa kupanua dola yake kuanzia greece mpaka egypty, huku akihamasisha vijana kuwa magavana na mageneral katika kila kona ya dola hiyo.Kijana huyu alitengeneza mpaka irrigation scheme kwa wakati huo ili vijana waweze kulima
Julius Nyerere akiwa na miaka 42 tu alikuwa kiongozi wa nchi hii na kwa mafanikio makubwa kabisa alihamasisha vijana wenzie kusoma na kushika uchumi wa nchi na akawapa kazi mbalimbali katika serikali yake, mfano mzuri ni DR. SALIM aliyeteuliwa kuwa balozi akiwa na miaka chini ya thelathini.
Wakati marekani ikiwa na population zaidi ya nusu vijana, wakamchagua kennedy akiwa na umri wa miaka 45 tu, kennedy anakumbukwa mpaka leo kwa mambo makubwa aliyofanya katika kipindi kifupi. Hasa katika sela zake zilizotoa kipaumbele kwa vijana
Pia baada ya kuchoswa na sela za kizee za BUSH yule mzee, wamerekani wakaona ni muhimu kumchagua kijana ili kuleta mabadiliko ya msingi, na hapo William Jefferson (Bill clinton) alichaguliwa akiwa na umri wa miaka 47 tu.Nani asiyejua jinsi Clinton alivyoshughulikia suala la ajira nchini marekani.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi