Skip to main content

WALAKA WA AMINA SANGA


MWANDISHI, AMINA SANGA.
Moja kati ya kosa ambalo watu wengi wanafanya/ walishawahi kuyafanya ni kutaka KUELEWEKA. Wengi wetu tumejikuta tunachelewa kufanya / kutimiza ndoto, mipango, vitu tunavyovitamani kwasababu ya kutaka kueleweka. Unataka kila mtu akuelewe Kwamba una mipango mikubwa, Kila mtu a appreciate, halafu inakuja kuwa kinyume na hivyo na unaishia kukata tamaa, kwasababu unataka tu ueleweke.
IPO HIVI, binadamu wengi huwa hawaelewi MCHAKATO. , ukiwa kwenye mchakato si rahisi watu kukuelewa, watu wanaelewa zaidi MATOKEO, na si ajabu yuleyule aliyekukatisha Tamaa akawa wa Kwanza kushangilia MATOKEO.

Lakini pia, sio kila unachokifanya watu wajue( keep them under low profile) Kwa usalama wako. Don't post everything, don't speak everything. Don't let them predict your future. Ukitaka kueleweka utajikuta unaishia hapohapo ulipo. Work hard in silence let success make noise (quoted)

Usimuamini kila mtu, usimuweke karibu kila mtu. Kuna vitu kaa navyo mwenyewe mpaka vitokee, wengine wangeshakua wamefanya vitu vikubwa, wengine wangekua wameandika vitabu vingi, hawachukui hatua kwasababu wanataka kueleweka. Usilazimishe watu wakuelewe, sio lazima. WE PAMBANA, You're the captain of your own ship.
Amina Sanga
Nguvu ya Uthubutu

Comments

  1. HAKIKA AMINA UMENIFUNDISHA KITU MUHIMU, NIKO DARASANI KUJITAFAKARI KWA MANENO HAYO HAPO JUU, NAHISI ITANICHUKUA MUDA ZAIDI KUURUDIA HUU UJUMBE MPAKA NIELEWE VIZURI KWA FAIDA YANGU NA YA WENGINE PIA

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi