Skip to main content

YOPOCODE

YOUTH POTENTIALS FOR COMMUNITY DEVELOPMENT (YOPOCODE)
Jina la shirika ni;
Youth Potentials for Community development YOPOCODE

Makao makuu yake ni mtaa wa Mazingula, kata ya Ilembo, Halmashauri ya wilaya ya Mbeya vijijini mkoani Mbeya nchini Tanzania. Na tayari YOPOCODE wana tawi Mkoa wa Singida.
Usajili wake:
Shirika letu limesajiliwa chini ya sheria ya taasisi zisizokuwa za kiserikali kifungu cha 24 ya mwaka 2002.
Eneo la kazi;
Shirika letu linafanya kazi nchi nzima isipokuwa visiwani Zanzibar.
Dhamira ya YOPOCODE ni kuwawezesha vijana kwa kuwajengea uwezo Wa kujitambua na kutumia rasilimali zinazo wazunguka na fursa mbalimbali zinazopatikana katika maeneo yao kwa lengo la kuleta maendeleo katika jamii.
Dira
Dira yetu ni kuwa shirika kubwa Tanzania litakalo wawezesha vijana kujitambua kwa kutumia uwezo walionao au vipaji au taaluma au rasilimali zinazo wazunguka ili kujiletea maendeleo katika jamii.
 MALENGO YA SHIRIKA LA VIJANA TANZANIA LA YOPOCODE:
1. Ni kutoa elimu itakayowajengea uwezo vijana Tanzania kutambua na kutumia fursa zilizopo katika Jamii zao kwa maendeleo yao na jamii yao.
2. Kuhamasisha uundwaji wa vikundi vya ujasiriamali na uchumi kwa vijana Tanzania.
3.kuwahamasisha vijana Tanzania kushiriki katika shughuli za maendeleo
4. Kutoa elimu ya uzazi na maambukizi ya ukimwi kwa vijana Tanzania.
5. Kuwachochea vijana Tanzania kushiriki na kukubali mabadiliko ya kisera na kushiriki katika utekelezaji kiuchumi kwa ajili ya maendeleo ya Jamii zao na taifa kwa ujumla Wake.
UWANACHAMA KATIKA SHIRIKA LA YOUTH POTENTIALS FOR COMMUNITY DEVELOPMENT YOPOCODE:
Shirika linawakaribisha watanzania wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea na wenye akili timamu kuwa wanachama wa shirika letu la youth potentials for community development (YOPOCODE)
AINA YA UWANACHAMA
Kuna aina Tatu za uwanachama katika shirika letu la YOPOCODE;
A) Wanachama waanzilishi
B) Wanachama wa kawaida
C) Wanachama wadhamini, washauri au walezi.
D) mabalozi wawakirishi wa YOPOCODE Tanzania.
HAKI ZA WANACHAMA WA YOPOCODE;
A) Kuomba na kupata ripoti za matumizi ya fedha na maendeleo ya shirika kwa mwaka.
B) kuhudhuria vikao Vyote vya shirika vilevilivyokubalika.
C) kupewa kadi ya uwanachama na nakala ya katiba Mara baada ya kulipa ada ya mwaka ya uwanachama.
WAJIBU NA KAZI YA MWANACHAMA KATIKA SHIRIKA
A) Kuhudhuria kikao cha wanachama wote cha mwaka
B) Kulipa ada ya mwanachama na michango mwingine itakayopendekezwa na kikao kikuu cha mwaka cha wanachama wote.
C) kujitolea kufanya kazi kulingana na malengo ya shirika.
KARIBUNI SANA WATANZANIA WENZANGU WENYE NIA YA DHATI KULISAIDIA TAIFA LETU NA VIJANA TANZANIA.

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi