Skip to main content

BARUA YA MWALIKO

BARUA YA MWALIKO KATIKA UZINDUZI RASIMI WA SHIRIKA LA VIJANA LA YOPOCODE
Ndugu/Mheshimiwa/ Daktari/Profesa/ Mr na Mrs............................
Kwa heshima ya pekee, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la vijana Tanzania la YOPOCODE anakualika katika uzinduzi rasimi wa shirika tajwa lenye namba za usajili ooNGO/0009193.

Uzinduzi utafanyikia yalipo Makao makuu ya YOPOCODE mtaa wa mazigula, kata ya Ilembo katika Halmashauri ya Mbeya vijijini tarehe 08/08/2017 kuanzia saa Tatu asubuhi hadi saa nane za mchana.
Uzinduzi utaenda sambamba na shughuli mbalimbali ikiwemo na harambee maalumu ya kuchangia fedha kwa ajili ya kuimarisha shughuli za shirika na kuwa mkombozi kwa vijana kwa Mkoa wa Mbeya na Tanzania kwa ujumla wake.
USHIRIKI WAKO NI MUHIMU SANA KATIKA TUKIO HILI LA KIHISTORIA, TUNAOMBA UFIKE BILA KUKOSA. AIDHA WAWEZA KUTOA MCHANGO WAKO WA HALI NA MALI KUFANIKISHA TUKIO HILI.
 KAMATI YA MAANDALIZI
 0758051641 ALFRED MWAHALENDE
 0768577408 INNOCENT LAIZER
KARIBUNI SANA

Comments

  1. Ni kweli kabisa mungu atupe nguvu ile sisi vijana tuwe chachu ya taifa na tutambue uzalendo wetu

    ReplyDelete
  2. Ni kweli kabisa mungu atupe nguvu ile sisi vijana tuwe chachu ya taifa na tutambue uzalendo wetu

    ReplyDelete
  3. Nashukuru Sana nilichokua sijui sasa nimepata kufahamu kuusu kijana Asante Sana mwalimu

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi