Skip to main content

KUHUSU KITABU CHA DIRA YA KIJANA TANZANIA

KUHUSU KITABU CHA DIRA YA KIJANA TANZANIA
Ni kitabu pekee kilichobeba elimu stahiki ya stadi za maisha kwa vijana na chenye ubora wa hali ya juu kinachochambua na kutoa dira ya safari ya maisha ya kijana na miongozo inayotoa ramani ya kumsaidia kijana kujisimamia  mwenyewe na kujiajiri  kwa kutumia fursa mbalimbali za ujasiriamali zilizopo kama vile uwekezaji katika sekta ya  viwanda, kilimo biashara, ufugaji wa kisasa, madini, biashara ndogo ndogo, za kati na kubwa zilizopo katika jamii na kuweza kuendesha shughuli za uzalishaji mali na maisha yao bila kutegemea usimamizi kutoka kwa mtu mwingine ( kuajiriwa).
Kitabu hiki ni chachu ya mabadiliko chanya kwa vijana na kinatoa hamasa na kuwachochea vijana kushiriki katika harakati za kuleta maendeleo katika jamii zao na kukubali mabadiliko ya kisera na kuacha kukaa vijiweni kulia na kulalamika juu ya hali ngumu ya kimaisha (vyuma vimekaza) na ukosefu wa ajira katika sekta za serikali na mashirika binafsi na badala yake washiriki kikamilifu katika zoezi la kuinua uchumi wao na uchumi wa nchi kwa ajili ya maendeleo yao na taifa kwa ujumla Wake.
Dhima ya kitabu hiki ni kuwawezesha vijana kwa kuwajengea uwezo wa kujitambua, kujiamini, kujithamini, kuthubutu, kujitegemea kifkira na kutumia rasilimali zinazo wazunguka na fursa mbalimbali zinazopatikana katika maeneo yao kama ardhi, vyanzo vya nishati, mito, misitu, madini, nguvu kazi na elimu kwa lengo la kuleta maendeleo yao binafsi na ya jamii zao.
Kutokutambua thamani ya kijana katika Taifa au jamii ni kushindwa kutambua mchango wake katika mapambano dhidi ya harakati za kuleta maendeleo chanya katika taifa. Taifa lolote duniani haliwezi kukua na kuwa imara kiuchumi, kisiasa, kitamaduni na kijamii bila  kuwajengea uwezo vijana kwa kuwapa Dira itakayotoa hamasa ya kushiriki  kikamilifu katika mapambano dhidi ya  changamoto zinazolikibili taifa lao kama njaa, vita, umaskini, maradhi, uhaba wa ajira, uwekezaji duni, kukosekana kwa nguvu kazi, elimu duni na ugumu wa maisha. Kwa hiyo kitabu hiki pekee ni nguzo imara ya dira ya kijana Tanzania.
     KUHUSU WAANDISHI
Hiki ni kitabu cha kwanza kwa ubora duniani kilichoandikwa kwa ustadi wa hali ya juu na waandishi vijana kutoka katika taaluma na fani mbalimbali zinazokidhi Nyanja zote za maisha ya binadamu kama Sanaa na Utamaduni, elimu ya ugunduzi wa vipaji na ubunifu, Sayansi ya Siasa, Biashara, Uchumi, Uongozi, Dini, Uandisi katika Idara ya Sayansi ya Komputa, Uandishi wa habari, utangazaji na mawasiliano, Ujasiriamali, Ualimu wa taaluma na Tehama na ustawi na maendeleo ya jamii.
Waandishi washiriki wa kitabu cha dira ya kijana ni Alfred Mwahalende, Adabert Chenche, Joas Yunus Buyungu (Jyb), Janerosa Mafwimbo, Hellen Mtui, Gasper Chacha,Jacob Mushi, Lazaro Samwel, Filbert Nyoni, Innocent Laizer, Angesta Nathanael, Deogratus Kessy,Mohammed Ismail Rwabukoba, Daniel Rwihula, Subira Mlaga, Nabe Rodrick Na Daktari Raymond Mgeni


Comments

  1. Nimefurahi kuona mmeshirikiana vijana wengi sana, hii inaashiria kupevuka kwa fikra za viajana wa kiafrika. Ushirikiano ukiwepo Afrika inaweza kuwa imara tena. Natarajia kazi nzuri kutoka kwenu makamanda.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi