Skip to main content

KAMPENI YA BINTI AMKA TANZANIA YAANZA RASIMI JIJINI DAR ES SALAAM.

KAMPENI YA BINTI AMKA TANZANIA YAANZA RASIMI JIJINI DAR ES SALAAM.
Yopocode kwa kushirikina na Mabalozi wa kampeni ya Binti Amka Tanzania wameanza rasimi kampeni katika shule ya Msingi Mnazi Mmoja iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jijini Dar es salaam.
Akizungumza kwa niaba ya shirika la vijana Tanzania la YOPOCODE, Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Alfred Sostern Mwahalende amekuwa na haya ya kusema"kampeni ya Binti Amka Tanzania inalenga kumsaidia mtoto wa kike nchini  kufika ndoto yake na malengo yake kielimu, kiuchumi na kiuongozi na katika hili pia tutalenga kupambana na masuala ya mimba na ndoa za utotoni ambayo kwa kiasi kikubwa yamekuwa yakichangia katika kumkwamisha mtoto wa kike kufikia malengo  yake.Tumeanza na shule za misingi katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jijini Dar Es Salaam huku tukifanya juhudi katika halmashauri zingine na mikoa mingine ambayo tayari tumeanza maandalizi ya kuzindua kampeni yetu"
Katika kuhakikisha tunafikia lengo la kampeni hii, tumependekeza kuwasilisha mada zifuatazo, Nafasi ya elimu kwa mtoto wa kike,Mbinu za kutimiza malengo yako, Thamani ya mtoto wa kike katika jamii, Kulijua Kusudi na Kutimiza Ndoto Yako,Nafasi ya mtoto wa kike katika maendeleo, Binti na Uongozi Katika Karne hii,Fursa zilizopo kwa mabinti katika nyanja za kimaisha,Athari ya mimba na ndoa za utotoni, Umuhimu wa kujua sera na sheria kwa mtoto wa kike,Nguvu na thamani ya kipaji, Elimu ya afya ya uzazi na maumbukizi ya ukimwi,Malengo endelevu ya dunia (SDGs).
Aidha kwa upande wake mkuu wa shule ya msingi ya Mnazi Mmoja Mwalimu Abdulaziz amepongeza timu ya mabalozi na shirika kuanzisha kampeni hii ambayo itakuwa msaada mkubwa kwa watoto wa jinsia zote ususani wa kike kujengewa uwezo wa kujitambua, kujiamini, kusimamia malengo yao,kujithamini na kuweka mikakati ya kuzifika ndoto zao.Ikumbukwe kama iliyo kwa watoto wa kiume pia watoto wa kike wana ndoto zao, hivyo ni jukumu la mabalozi wa kampeni ya binti amka Tanzania kuhakikisha wanasimama kideta kumkomboa mtoto wa kike.



Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi