Skip to main content

MABALOZI WA BINTI AMKA TANZANIA

Binti Amka Tanzania, ni kampeni inayoratibiwa na viongozi wa YOPOCODE kwa Kushirikiana na MABALOZI WA BINTI AMKA TANZANIA. Kampeni hii inalenga kumsaidia mtoto wa kike Tanzania kufikia malengo yake kielimu, kiuchumi na kiuongozi/kisiasa, inalenga kupambana na changamoto mbalimbali zinazomkwamisha mtoto wa kike kufikia ndoto zake ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, utoro wa masomo, mfumo dume katika jamii, kukosekana mahitaji na mifumo sawa kwa jinsia zote kupata fursa sawa na vipaumbele sawa.
kwa mjibu wa shirika la watoto duniani UNICEF kumekuwa na ongezeko kubwa la mimba mashuleni kutoka 23% hadi 26% yaani takribani watoto 8000 hapa Tanzania kila mwaka hukatisha masomo kwa ajili ya ujauzito na ndoa za utotoni ambazo kwa kiasi kikubwa huathiri ndoto zao za kielimu, kiuchumi na kisiasa.
 Vilevile idadi kubwa ya watoto wa kike wamekuwa wakimaliza elimu ya msingi lakini upoteza nafasi ya kujiendeleza kielimu hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kujiunga na sekondari nayo imekuwa ikiongezeka, pia kushuhudia kuongezeka kwa vitendo vya kikatili wa kingono kama ubakaji na ulawiti kwa watoto wakike na chakusikitisha zaidi vitendio hivyo vimekuwa vikifanywa na ndugu wa karibu sana wa watoto hawa wakiwemo wazazi,walezi, majirani na hata walimu uko mashuleni matukio haya yamekuwa hayaripotiwi kwenye vyombo vya sheria kwani mengi huzungumzwa kifamilia na kuwaacha watuhumiwa wakiendelea na maisha yao..
 Inasikitisha kuona kuwa mtoto wa kike hapa nchini bado wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi na cha kusikitisha zaidi mtoto huyu anaanza kubaguliwa kuanzia katika ngazi ya familia.Katika familia nyingi za kitanzania mtoto wa kike amekuwa akikosa fursa ya kupata Elimu ukilinganisha na mtoto wa kiume na katika mazingira mengine wazazi wamediriki hata kuwaozesha watoto wao wa kike kwa ajili ya kupata fedha ya kusomesha watoto wa kiume. Ukiangalia pia katika suala zima la Elimu ni ukweli usiofichika kuwa idadi ya wasichana wanaoshindwa kumaliza masomo kwa sababu za kupata mimba imekuwa ikiongezeka.
MAJUKUMU YA “MABALOZI  WA BINTI AMKA TANZANIA”
1. Kuhakikasha upatikanaji wa taarifa sahihi za mabadiliko yanayotokea katika mwili wa mtoto wa kike pindi anapovunja ungo.
2. Kutoa elimu ya kujitambua kupitia semina, makongamano na clubs mbalimbali zenye lengo la kumsaidia mtoto wa kike kufikia malengo yake kielimu, kiuchumi na kiuongozi
3. kuwawezesha MABINTI  kwa kuwajengea uwezo Wa kujitambua na kutumia rasilimali zinazo wazunguka na fursa mbalimbali zinazopatikana katika maeneo yao kwa lengo la kuleta maendeleo katika jamii.
4. Kuwahamasisha vijana wa kike kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kuwa sehemu ya mabadiliko na kujikwamua kiuchumi na kuondoa dhana tegemezi.
TANZANIA BILA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI INAWEZEKANA
TUSHIRIKI KATIKA KAMPENI YA BINTI AMKA TANZANIA KUMSAIDIA MTOTO WA KIKE KUFIKA MALENGO YAKE KIELIMU, KIUCHUMI NA KIUONGOZI

KARIBU UWE BALOZI WA KAMPENI YA BINTI AMKA TANZANIA “JIUNGE KWA WHATSAPP NO 0758051641



Comments