Skip to main content

MABALOZI WA BINTI AMKA TANZANIA

Binti Amka Tanzania, ni kampeni inayoratibiwa na viongozi wa YOPOCODE kwa Kushirikiana na MABALOZI WA BINTI AMKA TANZANIA. Kampeni hii inalenga kumsaidia mtoto wa kike Tanzania kufikia malengo yake kielimu, kiuchumi na kiuongozi/kisiasa, inalenga kupambana na changamoto mbalimbali zinazomkwamisha mtoto wa kike kufikia ndoto zake ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, utoro wa masomo, mfumo dume katika jamii, kukosekana mahitaji na mifumo sawa kwa jinsia zote kupata fursa sawa na vipaumbele sawa.
kwa mjibu wa shirika la watoto duniani UNICEF kumekuwa na ongezeko kubwa la mimba mashuleni kutoka 23% hadi 26% yaani takribani watoto 8000 hapa Tanzania kila mwaka hukatisha masomo kwa ajili ya ujauzito na ndoa za utotoni ambazo kwa kiasi kikubwa huathiri ndoto zao za kielimu, kiuchumi na kisiasa.
 Vilevile idadi kubwa ya watoto wa kike wamekuwa wakimaliza elimu ya msingi lakini upoteza nafasi ya kujiendeleza kielimu hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kujiunga na sekondari nayo imekuwa ikiongezeka, pia kushuhudia kuongezeka kwa vitendo vya kikatili wa kingono kama ubakaji na ulawiti kwa watoto wakike na chakusikitisha zaidi vitendio hivyo vimekuwa vikifanywa na ndugu wa karibu sana wa watoto hawa wakiwemo wazazi,walezi, majirani na hata walimu uko mashuleni matukio haya yamekuwa hayaripotiwi kwenye vyombo vya sheria kwani mengi huzungumzwa kifamilia na kuwaacha watuhumiwa wakiendelea na maisha yao..
 Inasikitisha kuona kuwa mtoto wa kike hapa nchini bado wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi na cha kusikitisha zaidi mtoto huyu anaanza kubaguliwa kuanzia katika ngazi ya familia.Katika familia nyingi za kitanzania mtoto wa kike amekuwa akikosa fursa ya kupata Elimu ukilinganisha na mtoto wa kiume na katika mazingira mengine wazazi wamediriki hata kuwaozesha watoto wao wa kike kwa ajili ya kupata fedha ya kusomesha watoto wa kiume. Ukiangalia pia katika suala zima la Elimu ni ukweli usiofichika kuwa idadi ya wasichana wanaoshindwa kumaliza masomo kwa sababu za kupata mimba imekuwa ikiongezeka.
MAJUKUMU YA “MABALOZI  WA BINTI AMKA TANZANIA”
1. Kuhakikasha upatikanaji wa taarifa sahihi za mabadiliko yanayotokea katika mwili wa mtoto wa kike pindi anapovunja ungo.
2. Kutoa elimu ya kujitambua kupitia semina, makongamano na clubs mbalimbali zenye lengo la kumsaidia mtoto wa kike kufikia malengo yake kielimu, kiuchumi na kiuongozi
3. kuwawezesha MABINTI  kwa kuwajengea uwezo Wa kujitambua na kutumia rasilimali zinazo wazunguka na fursa mbalimbali zinazopatikana katika maeneo yao kwa lengo la kuleta maendeleo katika jamii.
4. Kuwahamasisha vijana wa kike kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kuwa sehemu ya mabadiliko na kujikwamua kiuchumi na kuondoa dhana tegemezi.
TANZANIA BILA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI INAWEZEKANA
TUSHIRIKI KATIKA KAMPENI YA BINTI AMKA TANZANIA KUMSAIDIA MTOTO WA KIKE KUFIKA MALENGO YAKE KIELIMU, KIUCHUMI NA KIUONGOZI

KARIBU UWE BALOZI WA KAMPENI YA BINTI AMKA TANZANIA “JIUNGE KWA WHATSAPP NO 0758051641



Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi