Skip to main content

DIRA YA KIJANA TANZANIA

DIRA YA KIJANA TANZANIA
BY ALFRED MWAHALENDE
2017
Yaliyomo
I kijana ni nani?
2 ujana ni nini?
3 sifa na wajibu wa kijana
4 nafasi ya kijana katika maendeleo ya jamii
5 vijana kushiriki katika maendeleo ( fursa zilizopo Tanzania vijana kujiwekeza)
6 je, kijana ni taifa la leo au kesho?
7 mifano na historia ya vijana/vijana waliowahi kufanya vizuri
8 biashara, ujasiriamali na makundi ya ujasiriamali kwa vijana
9 changamoto zinzowakwamisha vijana katika kufikia ndoto zao
10 mipango na mikakati ya Tanzania mpya ya vijana.

Kijana ni nani?
Ø       Neno kijana linatafsiriwa katika tafsiri tofauti katika kila jamii, Mathalan nchini Tanzania kijana ni mtu mwenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 35, yaani baada ya balehe. Mabadiliko makubwa ya kimaumbile hutokea sambamba na kukomaa kwa mawazo.
Ø       Aidha Kwa mujibu wa sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15 hadi 24.
Ø       Hali kadhalika Kwa tafsiri ya umoja wa mataifa, Kijana ni mwanamke au mwanamme aliye na umri kati ya miaka 15 hadi 24. Tafsiri hii hutofatiana kutoka nchi moja hadi nchi nyingine. Nchi au maeneo mengine ya dunia huwa na tafsiri tofauti kulingana na mahitaji ya mazingira na maeneo yao, na pengine kwa mujibu wa mifumo ya kijamii,kisiasa na kisheria katika nchi hizo.
Ø       Katika mikataba na sheria mbalimbali za kimataifa zinafafanua kuwa binadamu mwenye umri kuanzia miaka 0-17 ni mtoto na haruhusiwi kufanya maamuzi yeyote mazito kuhusu maisha yake, ingawa kamusi tajwa hapo mwanzo inaleta utata katika vipande viwili vya umri hasa katika maana ya kijana,kamusi inasema kijana ni mwana mdogo,mtoto mwenye umri wa miaka 7 hadi12.
Ø        Lakini katika mtazamo wa kawaida tunaamini kuwa kijana ni binadamu mwenye umri wa

Ø       Kuanzia miaka 18-40 na wakati mwingine mpaka miaka 45. 

Comments

Popular posts from this blog

WITO NI NINI?

MJUE ALIYEKUITANA KUMTUMIKIA WITO NI NINI? Kila mtu Mungu amemwita kwa nafasi yake amtumikie.Hata kama kwa nje wito utaonekana kufanana haina maana wito wa mtu mmoja na mwingine unafanana. Wito unatokana na kuitwa. Kila mtu Mungu amemwita amtumikie katika eneo Fulani.  Wito : Ni sauti au agizo analosikia mtu likimwelekeza nini cha kufanya.Katika wito wowote ukiwa umeitwa na Mungu atakuelekeza nini cha kufanya.Na unapoitwa na Mungu jitahidi kutenda sawa na wito wako ulivyo. NITAJUAJE NIMEITWA? 1.Utaisikia sauti ya Mungu ikisema na wewe: Kama kuitwa kwa kawaida kulivyo ndivyo mtu uisikia sauti ya Mungu  ikisema nae. Ebu angali mifano ya watu mbalimbali waliowahi kuisikia sauti ya Mungu ikiwaita kwa ajili ya kutekeleza agizo fulani. MUSA kabla ya kuanza kumtumikia Mungu alikuwa mchungaji wa mifugo ya mkwe Yethro kuhani wa Midiani.Katikati ya uchungaji Mungu alimwita Musa.Kumbe ili na wewe umtumikie Mungu unatakiwa uisikie sauti yake ikisema na wewe,Ni hatari sana kama uta

KIJANA NI NANI???

KIJANA NI NANI? NA MWANDISHI,  JANEROSA MAFWIMBO Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24. Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. Tofauti kati ya mtoto na kijana, wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mtoto na kijana hasa waliopo katika elimu ya msingi na sekondari kutokana

MAMBO 12 YA KUFANYA UKIWA KIJANA

Vijana Tanzania Na Alfred Mwahalende Kwa mujibu wa mwandishi wa blog ya Dira Ya Kijana Tanzania  Janerosa Mafwimbo anasema “ Neno kijana limekuwa na maana pana na linakuwa likipata tafsiri mbalimbali kutoka katika kila Taifa, jamii au tamaduni fulani. Kwakuzingatia mifumo au maisha ya jamii tunapata baadhi ya tafsiri za neno kijana kama ifuatavyo: 1.     Kijana ni mtu wa miaka 15-24. Hii ni tafsiri ya umoja wa Mataifa. 2.     Mathalani nchini Tanzania kijana ni mtu wa miaka 18-35 yaani baada ya balehe na mabadiliko ya maumbile toka utoto kuelekea ukubwa, aidha kw mujibu wa sera ya Taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, inasema kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15-24.Hivyo basi kijana ni mtu yeyote wa kike au kiume mwenye umri wa miaka 18-35 ambaye kwa mujibu wa mifumo ya kijamii au kitamaduni, kisiasa na kisheria anauwezo wa kujitegemea na kufanya maamuzi yake binafsi. ” JE, UJANA NI NINI? 3.     Ujana ni hatua ambayo mtu anapi